• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali

Waziri Jafo, Aongoza Mawaziri utatuzi wa Mgogoro wa Hifadhi Makere kusini

Imewekwa tar.: January 7th, 2019

Mawaziri watano wakioongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Suleiman Jafo wamekagua hifadhi ya Msitu wa Makere Kusini, uliopo wilaya ya Kasulu mkoa wa Kigoma kwa takriban saa tano ili kubaini changamoto mbalimbali za msitu huo na kuzipatia ufumbuzi.

Mawaziri wengingine mbali ya Mhe. Seleman Jafo, ni Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Hamis Kigwangala, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk. Angeline Mabula pamoja na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Musa Sima.

Ziara ya mawaziri hao katika hifadhi ya msitu huo ambao pia unatambulika kama Msitu wa Kagera Nkanda ambao niwa kihistoria kutokea hapa nchini ilianza majira ya saa saba mchana jana wakati Mawaziri hao walipokuwa wakitokea wilayani Kigoma ambapo walikuwa na kikao cha utatuzi wa mgogoro wa matumizi ya ardhi katika hifadhi ya Msitu na Pori la Akiba la Moyowosi la mkoani Kigoma na kumalizika kwa ukaguzi majira ya saa kumi na mbili jioni.

Baada ya kumalizika kwa ukaguzi katika Msitu wa Makere Kusini, Mawaziri hao watano walielekea kijiji cha Kabulanzwili na kukagua mpaka baina ya kijiji hicho na hifadhi ya msitu huo kwenye mto Migezibiri na baadaye kukutana na wananchi wa kijiji hicho kwa lengo la kuwaeleza nia ya serikali kunusuru hifadhi ya msitu ambapo walizungumza nao hadi saa moja na nusu usiku.

Wakiwa katika kijiji cha Kabulanzwili waliwapokelewa na wananchi walikuwa na   mabango huku wananchi wakionesha kutoridhishwa na hatua zinazochukuliwa na askari wa wanyama pori katika eneo hilo kwa kuwaondoa kwa nguvu wananchi wanaoendesha shughuli za kilimo na ufugaji kwenye hifadhi hiyo, huku baadhi yao wakidai kutofahamu mipaka halisi baina ya kijiji na hifadhi katika eneo hilo.

Ziara ya viongozi hao ilikwenda sambamba na kufikia maazimio tisa kwa ajili yakunusuru misitu lakini pia kumaliza migogoro iliyokuwepo baina ya serikali na wananchi hao, maazimio yaliyofikiwa ni pamoja na;

Serikali itaendesha Operesheni kubwa kuondoa uvamizi wa wakulima, wafugaji na watu wengine wanaofanya shughuli zisizo halali kwenye misitu na mapori yaliyohifadhiwa kisheria zikiwemo hifadhi za misitu ya serikali kuu, hifadhi za misitu za halmashauri za wilaya na vijiji. Hivyo, wavamizi wote wanaoishi au kuendesha shughuli zozote kwenye mapori na misitu hiyo waondoke mara moja kwa hiyari kabla ya zoezi la kuwaondoa kwa lazima. Operesheni hiyo itafanyika wakati wowote ndani ya kipindi cha miezi sita (6) kuanzia Januari 2019. Hata hivyo, imeshauriwa kwa wakulima ambao tayari wana mazao katika mapori na hifadhi husika wanaweza kuomba idhini maalum ya kuvuna mazao yao.


Azimio linguine ni kwamba, Serikali imemega jumla ya hekta 10,012.61 kutoka kwenye Hifadhi ya Msitu wa Makere Kusini kwa ajili ya kilimo na mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu ambapo Hekta 2,174 (ekari 5,435) zimetolewa kwa Kijiji cha Mvinza, Hekta 2,496 (ekari 6,240) zimetolewa kwa Kijiji cha Kagerankanda na Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Hekta 5,342.61 (ekari 13,356.525). Eneo hili lilitolewa na Mhe. Rais ili litumike kwa ajili ya shughuli za kilimo na ufugaji. Serikali itaandaa mpango mahsusi wa matumizi bora ya ardhi ili kuwezesha zoezi la ugawaji kufanyika vizuri.


Taarifa iliyotolewa kwa umma imesema, Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetenga jumla ya hekta 20,000 kutoka katika maeneo mbalimbali katika Mkoa wa Kigoma kwa ajili ya ufugaji wenye tija aidha serikali itaendelea kutafuta maeneo mengine kwa ufugaji wenye tija.


Ilikuweka kuwa na msimamo wa pamoja Serikali imesisitiza kuimarisha utekelezaji wa sheria zinazohusu wakimbizi ili kuhakikisha hawachangii uharibifu wa mazingira, maliasili na usalama;

Maazimio mengine ni kuwa ilibainika wahamiaji haramu kutoka nje ya nchi wamekuwa wakichangia katika uharibifu wa misitu na mapori hivyo serikali imesema wahamiaji hao haramu wataondolewa nchini mara moja kwa kutumia sharia za nchi zilizopo.

Serikali imesema pia wananchi wote waliovamia eneo lililoko kwenye mpango wa uanzishwaji wa vitalu vya ufugaji na mashamba ya kilimo katika Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza (Mwanduhubanhu) watapangwa na mamlaka husika kwa ufugaji na kilimo chenye tija, mara baada ya tathimini iliyoelekezwa na Waziri wa Mifugo kukamilika;

Sambamba na hayo hapo juu, Serikali itasaidia vijiji katika maeneo yao kuandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi na katika mipango hiyo watenge maeneo kwa ajili ya ufugaji na kilimo kulingana na mahitaji yao;

Katika hatua nyingine maazimio hayo ya serikali kupitia Mwaziri wake, imesema, Mamlaka za Serikali za Mitaa zenye mashamba ambayo hayajaendelezwa zihakikishe taratibu za ubatilisho wa miliki hizo umefanyika ili ardhi itakayopatikana ipangwe kwa matumizi ya kilimo na ufugaji wenye tija huku iki utaka uongozi wa Mkoa na Wilaya uhakikishe kuwa usafirishaji wa mifugo unazingatia Sheria ya Utambuzi, Usajili na Ufuatiliaji wa Mifugo Na. 12 ya mwaka 2010.

Hii ni mara ya kwanza kwa Wizara hizo kukutana mkoani humo na kutafuta suluhu ya migogoro ya hifadhi hapa nchini.


Matangazo

  • ORODHA YA WAKUU WA KITENGO CHA FEDHA YENYE MABADILIKO 5-5-2022 May 06, 2022
  • Kazi za muda za makarani na wasimamizi wa Sensa 2022 May 05, 2022
  • MUDA WA NYONGEZA MAOMBI YA AJIRA ZA TAMISEMI 2022 May 04, 2022
  • Taarifa ya Kitengo Manunuzi na Ugavi, April 2022 April 04, 2022
  • Safeguard Documents for TACTIC Project March 30, 2022
  • Miongozo ya Operesheni Anwani za Makazi March 24, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • BARABARA YA MVUMI KUWEKWA LAMI KM 3

    May 26, 2022
  • PROF. SHEMDOE AZINYOOSHEA KIDOLE HALMASHAURI 8 KWA KUTOKUTENGE FEDHA ZA LISHE

    May 25, 2022
  • WAZIRI MKUU MAJALIWA ASIMAMISHA KAZI MKURUGENZI WA JIJI, MAAFISA WATANO ARUSHA

    May 24, 2022
  • WAKUU WA MIKOA SIMAMIENI UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO KWENYE HALMASHAURI

    May 24, 2022
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.