• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Tosiri aibuka kinara fainali za mita 200 Umisseta

Imewekwa tar.: June 15th, 2019


Na Mathew Kwembe, Mtwara

Mwanafunzi Ismail Hussein Tosiri kutoka shule ya sekondari Makongo ya jijini Dar es salaam, amefanikiwa kunyakua medali ya dhahabu kwa upande wa wavulana kwenye fainali za mashindano ya Umoja wa Michezo ya Shule za Sekondari (UMISSETA)  iliyofanyika leo katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara.

Ismail ambaye pia ni bingwa wa riadha kwa nchi za Afrika Mashariki kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 21 aliwaacha kwa mbali wanariadha wenzake Benedict Matias  kutoka Pwani ambaye alishika nafasi ya pili na Amos Charles  pia wa pwani ambaye alishika nafasi ya tatu.

Licha ya kukiri kuwa mashindano ya mwaka huu yalikuwa magumu kwake kutokana na ushindani wa hali ya juu uliojitokeza kwenye mbio hizo, Ismaili alijigamba kuwa siri ya mafanikio yake ni mazoezi makali aliyokuwa anayafanya kabla ya kuanza kwa mashindano hayo.

Amesema kuwa hivi sasa anajipanga vema ili aweze kufanya vizuri kwenye mashindano ya ya shule za Sekondari Afrika Mashariki FEASA yaliyopangwa kufanyika mkoani Arusha mapema mwezi wa nane mwaka huu.

 Kwa upande wa wasichana bingwa wa mbio za mita 200 ni Thereza Bernard kutoka Simiyu ambaye aliwashinda wenzake Emmy Hosea kutoka Singida aliyeshika nafasi ya pili na Hermegrida Manifred kutoka Pwani alishika nafasi ya tatu.

Katika fainali za mita 800, bingwa wa mbio hizo mwaka huu kwa upande wa wavulana ni mwanafunzi Japhet Joseph kutoka Singida ambaye alijinyakulia medali ya dhahabu, nafasi ya pili imeshikwa na Abrahamu Chapa wa Morogoro aliyejinyakulia medali ya fedha na medali ya shaba imekwenda kwa William Mguya kutoka Manyara ambaye alishika nafasi ya tatu.

Katika fainali za mita 800 wasichana, nafasi ya kwanza imechukuliwa na mwanariadha Gaudensia Manero kutoka mkoa wa Pwani, nafasi ya pili imechukuliwa na Rahel Nira wa Simiyu na nafasi ya tatu imekwenda kwa Regina Deogratius wa Pwani.

Kufuatia kukamilika kwa mbio hizo, mjumbe wa kamati ya ufundi wa chama cha riadha Tanzania Robert Kalyahe alisema kuwa wanariadha walioshindana katika mbio za mita 200 na 800 mwaka huu walishindwa kufikia viwango vya mwaka jana na miaka iliyopita kwa vile wengi wa waliokuwa wakishiriki mashindano hayo ni wapya kwa vile wazoefu wengi wamekwishamaliza elimu yao ya sekondari.

Kadhalika amesema kuwa wanafunzi wengi walioshiriki mbio hizo mwaka huu walikimbia bila ya kuwa na viatu jambo ambalo amesema kuwa siyo sawa kwani limewanyika ushindi vijana wengi waliokuwa na vipaji.

“Wanariadha walioshinda wengi wao walikuwa na viatu vya kukimbilia (spikes) ambavyo kariakoo bei yake haizidi shilingi 30,000, ukilinganisha na viatu vinavyotumiwa na wacheza mpira wa miguu ambavyo ni karibu shilingi 90,000, “ amesema Kalyahe, na kuongeza:

“Jamii inapaswa kuwekeza kwenye mchezo wa riadha kama kweli tunataka kurudisha heshima ya mchezo huu kama ilivyokuwa miaka ya nyuma ya ushiriki wa kina Nyambui, na Bayi.”

Kalyahe amesema kama kweli tunataka kushinda kimataifa jukumu la kutafuta vipaji vya wanamichezo wanariadha linapaswa kwenda hadi vijijini badala ya kuishia kwenye akademi za michezo.

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.