• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Serikali yawataka Maafisa Elimu kuleta mageuzi

Imewekwa tar.: September 17th, 2018

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe amesema pamoja na juhudi ambazo serikali inafanya, sekta ya elimu imeshindwa kuleta mageuzi ambayo serikali na wananchi wanayategemea.

Mhandisi Iyombe aliyasema hayo jana  kwenye kikao kazi maalumu kwa watendaji wa elimu katika ngazi ya taifa, mikoa na halmashauri kinachofanyika kwa siku mbili jijini Dodoma.

 “Mwaka 2015 watanzania walipiga kura kwa kutaka mabadiliko, mpaka sasa sekta ya elimu hakuna mabadiliko yaliyofikiwa tofauti na sekta ya afya, bado akili zenu zimelala pale pale,” alisema.

Aliongeza: “Watumishi wasiotaka mabadiliko waondoke wenyewe na kama hawataki kuondoka tutawaondoa hatuwezi kulazimisha mtu kufanya kazi kimazoea na ndiyo maana wengine wanataka kuhonga ili wapate nafasi badala ya kufanya kazi sawasawa.”

Alisema anachukuziwa na kuona mambo hayaendi vizuri kwenye sekta ya elimu wakati maofisa wa elimu ngazi ya mikoa, wilaya na kata wapo na kuonya kuwa endapo kuna kiongozi anaona haweza kuwa chachu wa mabadiliko katika eneo lake basi kiongozi huyo hatoshi.

“ Kuna mambo mengi mabaya yanatokea katika sekta ya elimu lakini viongozi nyinyi mpo tu na hakuna hatua yeyote mnayochukua huku mkisubiri maamuzi kutoka makao makuu.”
Mhandisi Iyombe alitolea mfano tukio la kuchapwa viboko hadi kufa kwa kwa mwanafunzi wa shule ya msingi Kibeta katika Manispaa ya Bukoba ambapo taarifa hiyo aliipata kutoka kwa mdhibiti wa ubora wa elimu wakati maafisa elimu mkoa, wilaya, kata wapo.

“Hakuna tukio baya na la kinyama kama lililofanywa na mwalimu wa shule ya Msingi Kibeta wilayani Bukoba lakini hakuna ripoti zozote zilizotolewa na wahusika na badala yake taarifa ilitolewa na Ofisa Uhakiki Ubora, wakati mwalimu mkuu yupo, afisa elimu kata, wilaya na mkoa wapo na unapowauliza wanasema eti ni tukio kubwa litaonekana kwenye vyombo vya habari yaani Mimi katibu mkuu nifanye kazi na kupeleka taarifa kwa Mheshimiwa Rais kupitia vyombo vya habari wakati uongozi upo kweli nyie mnatosha?” alihoji Mhandisi Iyombe

 Alisema kutowajibika ipasavyo kwa viongozi hao kumechangia hata tabia ya uvujaji na uwizi wa mitihani unaofanywa na baadhi ya shule kwa lengo la kujipatia umaarufu, lakini hakuna hatua zozote zinazochukuliwa.

Aidha, Katibu Mkuu amewataka viongozi hao ambao kwa nyadhifa zao wanaingia kwenye vikao vya maamuzi kuhakikisha wanajenga hoja za nguvu ili halmashauri zitenge fedha kwa ajili ya miundombinu ya shule katika eneo husika.

“ Mnapata nafasi ya kuingia kwenye vikao vya halmashauri, msiende huko kusinzia, mwende mkajenge hoja ili halmashauri zitenge fedha za ndani kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya shule maana wewe ndio unajua hali ya shule zako,” alisema.

Aliongeza: “ Kataeni kuwa na shule za nyasi, watoto wanakaa chini wakati kuna fedha za ndani za halmashauri zipo na kuna maeneo halmashauri zina mapato mengi ya ndani.”

Anaandika Mathew Kwembe- OR TAMISEMI


Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • TUNZENI VIFAA VYA AFYA VILIVYONUNULIWA NA SERIKALI - DKT. MAHERA

    March 30, 2023
  • REJESHENI MIKOPO ILI WENZENU WAPATE KUKOPA –KAMATI YA LAAC

    March 31, 2023
  • LAAC YARIDHISHWA NA USIMAMIZI WA UKARABATI SHULE YA SEKONDARI WASICHANA MTWARA

    March 31, 2023
  • KAMATI YA LAAC YAKAGUA MADARASA 7 YALIYOJENGWA KWA MAPATO YA NDANI NA NGUVU ZA WANACHI - MANISPAA YA SUMBAWANGA

    March 31, 2023
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.