• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Serikali kujenga Hospitali 67 mpya

Imewekwa tar.: July 12th, 2018

Serikali imetenga kiasi cha fedha shilingi bilioni105 za kitanzania kwaajili ya ujenzi wa Hospitali 67 za Wilaya katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2018/19 ili kuiwezesha kuwa na jumla ya Hospitali 137 za Wilaya ambazo zitasaidia kuimarisha hali ya utoaji wa huduma za afya nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo aliyasema hayo akiwa ziarani mkoani Singida katika Halmashauri ya Manyoni alipofika kukagua maendeleo ya ujenzi wa kituo cha Afya Kintinku katika Halmashauri hiyo ambacho kilikuwa miongoni mwa vituo vya mwanzo vilivyo pokea shilingi milioni 500 za kitanzania katika awamu ya kwanza ya ukarabati wa vituo vya afya 210 kote nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo mara baada yakujionea miundombinu mbali mbali iliyo jengwa na mingine kukarabatiwa ikiwepo Jengo la Upasuaji, Wodi ya Mama na Mtoto, Maabara, Jengo la kuhifadhia Maiti pamoja na Nyumba ya Mtumishi, Waziri Jafo alisema mara baada yakufanya kazi kubwa katika vituo vya afya nguvu kubwa sasa inahamishiwa katika Hospitali za Wilaya.

“Toka tupate uhuru nchi yetu ilikuwa na Hospitali 70 tu za wilaya zinazo milikiwa na serikali ikilinganishwa na idadi ya Halmashauri tulizo nazo sasa 185 utaona kabisa bado tunao uhitaji, hivyo Mhe. Rais anakwenda kuweka historia kwa kujenga Hospitali mpya 67 za Wilaya katika kipindi cha muda mfupi” alisema Waziri Jafo na kuongeza kuwa hayo ni mafanikio makubwa katika historia ya nchi yetu.

Mbali na kuelezea mipango ya Serikali katika kuboresha huduma mbali mbali ikiwepo suala la afya nchini, Waziri huyo vilevile aliwahimiza wananchi kujiunga na mfuko wa Afya ya jamii iliyo boreshwa (Improved Community Health Fund ICHF) ili waweze kupata matibabu kwa wepesi lakini pia kuiwezesha serikali kuimarisha huduma za afya kwakuwezesha upatikanaji wa madawa pamoja vifaa tiba vingine.

“Ndugu zangu hapa kijijini ukiuza kuku wako Majogoo wawili watakuwezesha wewe na familia yako kupata matibu ndani ya mwaka mzima kwa kiasi cha Tsh.30,000 tu hivyo niwaombe mlione hilo na mchukue hatua” alinukuliwa Waziri Jafo.

Katika hatua nyingine Waziri pia aliwataka wanachi wa Vijiji vinavyozunguka na kupatiwa  huduma katika kituo cha Afya Kintinku na sehemu zingene nchini kuwa walinzi wa miundombinu ya afya katika vituo hivyo ili viweze kutoa huduma za afya kwa muda mrefu.

Halmashauri ya Manyoni ni miongoni mwa Halmashauri zilizopatiwa fedha za ukarabati wa vituo vya afya vya Kintinku na Nkonko, ambapo katika awamu ya kwanza walipatiwa shilingi milioni 500 za kitanznia zilizo fanya ukarabati katika kituo cha afya Kintinku na katika awamu ya tatu Halmashauri hiyo imepelekewa kiasi cha shilingi milioni 400 za kitanzania kwa ajili ya ukarabati wa kituo cha Afya Nkonko, ukarabati unaotazamiwa kuchukua muda wa wiki 20 hadi kukamilika kwake.

Anaandika Atley Kuni- OR TAMISEMI

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.