• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)
    • Machaguo Kidato cha 5 & Vyuo

Serikali kuajiri waalimu 12,000 shule za Msingi na Sekondari

Imewekwa tar.: August 4th, 2020



Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amesema Serikali inaendelea na taratibu za kuajiri walimu 12,000 wapya kwa Shule za Msingi na Sekondari na zitakapokamilika zitatangazwa.

Ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza kwenye siku ya TAMISEMI ya kueleza mafanikio yaliyopatikana kwa kipindi cha miaka mitano katika sekta ya elimu iliyofanyika katika ukumbi wa  shule ya Sekondari Dodoma.

Amesema kuwa kwa kipindi cha miaka mitano walimu zaidi ya 18,000 wameajiriwa na kupelekwa Shule za Msingi na Sekondari na kwamba ajira zingine 12,000 zilizoelekezwa na Rais John Magufuli bado taratibu zake zinaendelea.

“Nafahamu bado kuna changamoto ndio maana Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli  ametoa maelekezo ya kuongeza ajira za walimu  na ametoa maelekezo ya ajira zaidi ya 12,000 taratibu zinaendelea zikikamilika Serikali itaongeza  ajira zingine kwa shule za msingi na sekondari,”amesema Mhe. Jafo.

Akizungumzia kuhusu mafanikio yaliyopatikana kwa miaka mitano katika Sekta ya Elimu ya Msingi na Sekondari Mhe.Jafo amesema katika kipindi hicho kiasi cha Sh.Trilioni 1.09 zimetolewa kwa ajili ya elimu bila malipo.

Amefafanua kuwa  kuwa zaidi ya Sh.Bilioni 502 zimetolewa kwa ajili ya elimu ya Shule za Msingi na Sh.Bilioni 593.9 zimeenda sekondari, jambo ambalo limesaidia watoto wa maskini kupata elimu.

“Mwaka 2016 watoto wengi walifurika kwenye shule zetu wakati zikiwa zimekadiria watoto 200 hadi 400, zingine ziliweza kusajili hadi wanafunzi 1,000, kwa mfano shule ya Nyakanazi na Majimatitu na watoto wengine walisajiliwa wakiwa na miaka 10 kutokana na miaka mitatu nyuma walikosa fursa hiyo,”amesema Jafo.

Ameendelea kufafanua kuwa  katika kipindi cha miaka mitano zaidi ya Sh.Bilioni 501 zimetolewa kwa ajili ya kuboresha miundombinu mbalimbali na hadi kufikia mwezi Juni 2020 ujenzi wa shule mpya za Msingi 905 zilikuwa zimekamilika hivyo  kuongeza idadi ya shule za Msingi kutoka 16,899 mwaka 2015 hadi 17,804 mwaka 2020.

Pia amesema  vyumba vya madarasa 17,215 vimejengwa na kuongezeka kutoka vyumba 108,504 mwaka 2016 hadi 125,719 mwaka 2020, sawa na ongezeko la asilimia 13.7 ambapo ujenzi wa vyumba 3,049 unaendelea na ukikamilika idadi ya vyumba vya madarasa kwa shule za Msingi itafikia 128,768.

Aidha, amesema serikali imejenga shule mpya za Sekondari 228 na hivyo kuongezeka kutoka shule 4,708 mwaka 2016 hadi 5,330 mwaka 2020.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tamisemi, Mhandisi Joseph Nyamhanga, amesema uwekezaji na maboresho yaliyofanyika katika sekta ya elimu kwa shule za msingi na sekondari umesaidia kuongeza kiwango cha ufaulu katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi kutoka asilimia 67.84 mwaka 2015 hadi asilimia 81.50 mwaka 2019.

Naye, Naibu Katibu Mkuu, Tamisemi anayeshughulikia Elimu, Gerald Mweli, amesema  Mpango wa Elimu bila malipo ulianzishwa mahsusi baada ya utafiti walioufanya mwaka 2014 kuonyesha kuwa Watoto milioni 3.5 wapo nje ya Shule kutokana na kukosa ada.

Na Angela Msimbira OR-TAMISEMI

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • TANGAZO LA KAZI - TOA July 22, 2022
  • MAJINA YA WALIOPATA AJIRA KADA ZA AFYA NA UALIMU June 26, 2022
  • ORODHA YA WAKUU WA KITENGO CHA FEDHA YENYE MABADILIKO 5-5-2022 May 06, 2022
  • Kazi za muda za makarani na wasimamizi wa Sensa 2022 May 05, 2022
  • MUDA WA NYONGEZA MAOMBI YA AJIRA ZA TAMISEMI 2022 May 04, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Utekelezaji wa Miradi ya Elimu isimamiwe na kukamilika kwa wakati- Dkt. Msonde

    August 15, 2022
  • UBUNIFU KIVUTIO UMISSETA 2022

    August 15, 2022
  • Bilioni 776.6 zaelekezwa katika ujenzi, ukarabati na matengenezo ya barabara vijijini na mijini katika mwaka wa fedha 2022/23

    August 14, 2022
  • TARURA KUONGEZA MTANDAO WA BARABARA ZA LAMI KM 1,450, CHANGARAWE KM 73,242’ ENG. SEFF

    August 14, 2022
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.