• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Jafo ataka nchi za Afrika Mashariki ziwe na mkakati wa pamoja kuendeleza vipaji vya Wanamichezo

Imewekwa tar.: August 16th, 2019

Na Mathew Kwembe, Arusha

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo amelitaka Shirikisho la Michezo kwa shule za Sekondari za Afrika Mashariki (FEASSSA) kuwa na mipango ya pamoja ya kuendeleza vipaji vya watoto vinavyoibuliwa kupitia mashindano ya FEASSSA.

Akifungua mashindano hayo leo kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha, Mhe.Jafo amesema lazima viongozi wa michezo kutoka nchi wanachama za Afrika Mashariki kuhakikisha kuwa wabnakwenda kuvilea vipaji vya wanamichezo vitakavyopatikana kupitia mashindano hayo.

Amesema kuna tabia imejengeka kwamba watoto wenye vipaji wanaibuliwa kupitia michezo hiyo lakini vipaji hivyo vinapotea kwa kukosa matunzo na hivyo kupotea.

“Niwaombe nchi wanachama kila mmoja katika nchi anayotoka twende tukavilee vipaji mbalimbali vitakavyoibuliwa  kupitia mashindano hayo,” amesema na kuongeza:

“Ninaamini tukifanya hivyo tutatenda haki sawa na changamoto kubwa ipo kwa wasichana ambapo taarifa zinaonyesha kuwa vijana wengi mahiri wasichana licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa kimichezo lakini mdondoko umekuwa ni mkubwa.”

Mhe.Jafo amewataka waratibu wa nchi mbalimbali zinazoshiriki michezo hiyo kwenda kuwalea vijana wenye vipaji ili kuweza kuendeleza vipaji vya vijana hao kwa maendeleo ya michezo katika nchi zao.

Amesema jukumu la viongozi wa jumuiya ya Afrika Mashariki katika sekta ya michezo ni kuhimiza na kuwajengea mazingira rafiki vijana ili waweze kukuza vipaji vyao na kujiendeleza katika michezo, kutanua wigo wao wa ushindani ndani na nje ya nchi, kanda na bara la Afrika.

Aidha Waziri Jafo amewataka wanamichezo wanaoshiriki michezo hiyo ngazi ya kanda kudumisha nidhamu wakati wote wa mashindano hayo.

“Mtambue kuwa nidhamu ina mchango mkubwa katika mafanikionkatika michezo na maisha kwa ujumla. Katika kushindana mtambue kuwa kuna kushinda na kushindwa,” amesema.

Pia amewataka vijana hao kuitumia fursa hiyo ya kukutana na wenzao kutoka nchi nyingine za Afrika Mashariki kubadilishana uzoefu wa masomo pia kwa ajili ya kuinua taaluma zao.

Waziri Jafo amewataka viongozi kutoka nchi za Afrika Mashariki wanaoshiriki mashindano hayo ya FEASSSA kuitumia fursa hiyo ya kuwepo nchini kuona uwezekano wa kutembelea vivutio mbalimbali vinavyopatikana nchini hususani kutembelea mlima Kilimanjaro na mbuga za wanyama za Tarangire na Ngorongoro ambazo zinapatikana katika mkoa wa Arusha kunapofanyikia mashindano hayo mwaka huu.

Mapema Rais wa FEASSSA Justus Mugisha  amesema nchi za Afrika Mashariki hazina budi kuweka misingi mizuri ya michezo shuleni ili ziweze kufanya vizuri katika mashindano ya kimataifa.

Amesema hatua ya nchi za Afrika Mashariki kupeleka nchi nne katika mashindano ya AFCON yaliyomalizika hivi karibuni nchini Misri ni dalili njema kuwa nchi hizo zimejipanga kufanya vizuri katika mashindano yajayo ya kimataifa.

“Ni lazima tuwekeze katika michezo kwa vijana kama hawa wanaoshiriki mashindano ya FEASSSA kama kweli tunataka kupata mafanikio kwenye michezo ya kimataifa,” amesema.

Naye Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Elimu bwana Tixon Nzunda jumla ya wanamichezo 3500 kutoka mataifa ya Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Sudani na wenyeji Tanzania bara na Zanzibar watashiriki michuano hiyo huku nchi ya Malawi ikishiriki michuano hiyo kama mwalikwa.

Amesema kuwa mashindano hayo yatashirikisha michezo ya soka, riadha, netiboli, mpira wa mikono, mpira wa mikapu, vinyoya, raga, mpira wa magongo, mpira wa meza, na mpira wa kengele.

Bwana Nzunda ameongeza kuwa malengo ya mashindano hayo ni kukuza fani za michezo kwa wanafunzi kwa kuwashindanisha ili kubaini vipaji vya wanafunzi kutoka nchi za Afrika Mashariki na pia kudumisha na kuendeleza mshikamano kwa nchi wanachama miongoni mwa wanafunzi, walimu na viongozi wa shule kutoka Afrika Mashariki.

Mara baada ya ufunguzi rasmi wa mashindano hayo, kulifanyika mchezo wa kwanza wa soka wavulana baina ya timu ya soka ya Lindi ambao walikuwa washindi wa tatu wa UMISSETA mwaka 2019 ambayo ilicheza na  mabingwa wa mashindano kama hayo wa nchini Kenya timu ya St.Antony ya Trans zoia ambapo matokeo yalionyesha mabingwa hao wa Kenya waliibugiza Lindi kwa magoli 4 kwa 0.

Michezo hiyo itaendelea kuchezwa kila siku hadi tarehe 24 agosti, 2019 ambapo fainali za michezo hiyo zitafanyika.

Ufunguzi wa mashindano hayo pia ulishuhudiwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.Mrisho Gambo na viongozi wa ngazi mbalimbali kutoka mkoa wa Arusha na nchi wanachama wanaoshiriki mashindano hayo.

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • TUNZENI VIFAA VYA AFYA VILIVYONUNULIWA NA SERIKALI - DKT. MAHERA

    March 30, 2023
  • REJESHENI MIKOPO ILI WENZENU WAPATE KUKOPA –KAMATI YA LAAC

    March 31, 2023
  • LAAC YARIDHISHWA NA USIMAMIZI WA UKARABATI SHULE YA SEKONDARI WASICHANA MTWARA

    March 31, 2023
  • KAMATI YA LAAC YAKAGUA MADARASA 7 YALIYOJENGWA KWA MAPATO YA NDANI NA NGUVU ZA WANACHI - MANISPAA YA SUMBAWANGA

    March 31, 2023
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.