• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Jafo apiga marufuku uchimbaji wa mchanga kwenye mito ya Dar es salaam

Imewekwa tar.: April 20th, 2018

Na Raphael Kilapilo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhe Selemani Jafo (Mb) amepiga marufuku uchimbaji wa mchanga unaoendelea katika mito mbalimbali Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Jafo alitoa katazo hilo wakati wa ziara yake ya kuangalia athari zilizotokana na mafuriko ambapo katika  barabara za mwendokasi eneo la Jangwani na  Manispaa ya Ilala leo tarehe 20 Aprili 2018.

Akiwa katika kata ya Gongolamboto eneo la Ulongoni A na Ulongoni B, alijionea jinsi ambavyo mafuriko yaliyotokana na wingi wa mvua zilizonyesha yalivyoharibu madaraja na kuacha athari kubwa kwa wananchi.

“Nimejionea mwenyewe jinsi ambavyo mvua hizi zimeleta athari kubwa hapa na kusababisha mawasiliano kukatika baina yenu nyinyi na wenzenu wa upande wa pili. Lakini niwaambie kuwa kwa sehemu kubwa baadhi ya wananchi wanachangia uharibifu wa maeneo haya kutokana na uchimbaji wa mchanga unaoendelea na kusababisha uharibufu katika kingo za mito pamoja na miundombinu hii iliyojengwa,” alieleza Mhe. Jafo

“Hatuwezi kuzizuia mvua zisinyeshe lakini hatuwezi kuvumilia kuwaacha watu wanaoharibu miundombinu na kingo za mto kwa kuchimba mchanga. Hivyo kuanzia leo napiga marufuku uchimbaji wa mchanga katika maeneo yote ya mito ya Dar es Salaam,” aliagiza Waziri Jafo.

Waziri aliendelea kueleza kuwa miundombinu inajengwa kwa gharama kubwa na Serikali lakini wapo watu ambao wanaiharibu kwa makusudi kutokana na uchimbaji wa mchanga, hivyo akaeleza kuwa Serikali haitavumilia swala hilo.

Alimuagiza Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Sofia Mjema aliyeambatana naye katika ziara hiyo kusimamia agizo hilo pamoja Mkoa wa Dar es Salaam kwa ujumla wake, na akaagiza kuwakamata wale wote watakaokaidi agizo hilo.

Aidha Mhe. Jafo alieleza kuwa Serikali inajitahidi kurejesha mawasiliano katika maeneo hayo yaliyoathirika kwa kujenga madaraja ya muda wakati wakisubiri ukarabati mkubwa kufanyika.

Alieleza kuwa amewasiliana na Waziri wa Ulinzi Mhe. Hussein Mwinyi ili Jeshi la Ulinzi lisaidie katika kutengeneza madaraja hayo.

“Waziri wa Ulinzi ameniahidi kuwa anatuma wataalamu wa Jeshi kufanya tathmini ya uharifu ili kutengeneza madaraja hayo ya muda,” alisema Jafo.

Awali, katika ziara hiyo Mhe. Jafo alitembelea Mradi wa Mabasi Yaendayo Kasi “DART” katika kituo cha Jangwani na kuangalia athari zilizoltokana na mafuriko.

Akiwa katika kituo hicho cha Jangwani alipongeza uongozi wa UDART kwa kuzingatia agizo lake alilolitoa awali la kuyahamisha mabasi katika kituo hicho na kuyalaza Kimara pamoja na Gerezani hivyo kufanikiwa kuokoa mabasi hayo.

“Mmeniambia kuwa yale mabasi niliyoyaona hapa wakati wa mafuriko ni yale ambayo yalikuwa hayatembei kabisa na hata hivyo mmetoa vifaa amabavyo vingeharibika katika mabasi hayo na mengine yote mliyatoa hapa. Nawapongeza kwa hilo,” alieleza Jafo.

Mhe.Jafo alisema kuwa mafuriko hutoke duniani kote marekani, china na kwingineko na hatuwezi kuyazuia, lakini ni akasema kuwa ni lazima wadau na wananchi wote wazingatie tahadhari zinazotolewa ikiwa ni pamoja na kuhama mabondeni ili kupunguza athari.

Pia alieleza kuwa Serikali inampango mkubwa wa kuutengeneza Mto Msimbazi kupitia Mradi wa DMDP, ambapo takribani dola za kimarekani 20 milioni zimetengwa ili kupata suluhisho la kudumu. Alieleza kuwa kazi hiyo inatarajiwa kuanza mwezi Septemba, 2018 mara baada ya kumalizika kwa usanifu.

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.