• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Hati Safi zimeongezeka katika Mamalaka za Serikali za Mitaa

Imewekwa tar.: April 13th, 2018
Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo amesema katika Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali, Halmashauri zilizopata Hati Safi zimeongezeka  kutoka Halmashauri 81 kwa mwaka 2015/16 mpaka kufikia Halmashauri 166 (90%) kwa mwaka  2016/17.

Jafo ameyasema hayo wakati kwa Kikao na Waandishi wa Habari kilichofanyika katika ukumbi Bunge kuhusu utekelezaji wa baadhi ya mapendekezo ya CAG kwa hesabu za Mamlaka za Serikali  za Mitaa kwa  mwaka Ulioishia  Juni 30, 2017.

Alisema “napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Wenyeviti na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kwa maelekezo yao mazuri yaliyosaidia sana utendaji kazi wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mikoa na MSM; Michango yao, ushauri na maelekezo yamewezesha kuongeza Idadi ya Hati Safi.

Akizungumzia kuhusu hoja zilizobainishwa katika ropoti ya CAG Mhe. Jafo alisema tumefanyia kazi mapendekezo yote yaliyotolewa katika ripoti zilizopita ambapo watumishi 434 wamechukuliwa hatua baada ya kubainika kusababishia halmashauri zao hasara/hoja zisizo za lazima kutokana na kutotekeleza ipasavyo wajibu wao ama kujihusisha na vitendo vya ubadhirifu.

“Kati ya hao 9 wamefukuzwa kazi, Watumishi 210 wamepewa barua za onyo huku Watumishi 15 wakifikishwa kwenye vyombo vya dola. Watumishi 28 wamesimamishwa kazi, 13 wametakiwa kufidia hasara kutoka kwenye mishahara yao wengine 4 wameshushwa vyeo na wengine 10 wamebadilishiwa majukumu” alisema Jafo.

Aliongeza kuhusu MSM kupokea Fedha pungufu ya Bajeti Iliyoidhinishwa ni kwa sababu Serikali hutegemea makusanyo ya mapato kutoka vyanzo mbalimbali. Hivyo, kiasi kinachotumwa kwenye MSM hutegemea mwenendo wa mapato yaliyopatikana lakini pia fedha za miradi ya maendeleo zilizotolewa na Serikali kwa mwaka wa fedha uliotaguliwa 2016/17 zimeongezeka ikilinganishwa na mwaka  wa 2015/16.

Kwa  mwaka 2016/17 fedha za miradi ya maendeleo zilizopokelewa na MSM ni Tsh. 705,927,921,596.20 sawa na 57% ya bajeti iliyoidhinishwa ya Tsh. 1,242,616,839,000 akati mwaka 2015/16, fedha zilizopokelewa  zilikuwa ni Tsh. 390,525,992,297 sawa  39%  ya bajeti ya Tsh. 1,010,650,744,099.

Kuhusu changamoto katika Usimamizi wa Mapato katika Mhe. Jafo alieleza Wizara imeendelea kuziba mianya ya uvujaji wa mapato kwa kuhakikisha kuwa Halmashauri zinahamia katika matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa ukusanyaji wa mapato ujulikanao kama Local Government Revenue Collection and Information System (LGRCIS) ambapo takwimu zote za mapato zinatunzwa katika mfumo huo ambao pia umeunganishwa na mashine za kukusanyia mapato (Point of Sales) zinazotumiwa na Mawakala/Wakusanya mapato, na hivyo kuiwezesha Halmashauri kufahamu mapato  yaliyokusanywa na Wakala/Wakusanya mapato hao.

Vile vile, mfumo huo umeunganishwa na mifumo ya benki, na hivyo kuwezesha Halmashauri kufahamu kiasi ambacho Wakala/Mkusanya mapato amekiingiza kwenye akaunti ya benki ya Halmashauri ikilinganishwa na kiasi alichokusanya. Mpaka sasa, Halmashauri zote 185 tayari zimewekewa mfumo huu wa LGRCIS.

Wakati huo huo alieleza Kuhusu Vitabu 379 vya Kukusanyia Mapato ambavyo havikuwasilishwa kwa Wakaguzi amesema  Licha ya kuwa  idadi ya Halmashauri na idadi ya vitabu vya kukusanyia mapato ambavyo havikuwasilishwa kwa Wakaguzi imepungua kutoka  871 katika Halmashauri 57 kwa mwaka 2015/16 mpaka vitabu 379 katika Halmashauri 21 kwa Mwaka 2016/17, OR – TAMISEMI imeendelea kusimamia maelekezo ya Serikali ya Halmashauri zote ziachane na ukusanyaji wa mapato kwa kutumia stakabadhi/vitabu vya kuandikwa kwa mkono, na badala yake mapato yakusanywe kwa kutumia mashine za kielektroniki.

Waziri Jafo alimalizia kwa kutolea ufafanuzi wa Soko la Mwanjelwa –Mbeya na kusema kuwa OR-TAMISEMI imeanza kuchukua hatua kuhusiana na dosari mbalimbali zilizojitokeza katika ujenzi wa soko la Mwanjelwa na kwa kuanza tulimuomba CAG kufanya ukaguzi maalum na taarifa iliashiria makosa ya kijinai na tayari Serikali imelifikisha suala hili kwenye vyombo vya Dola, ambapo pia Wahusika Wakuu wa mikataba husika na usimamizi wa utekelezaji wake, nao pia wameshafikishwa kwenye vyombo vya Dola kwa ajili ya uchunguzi na hatua zaidi. Serikali itaendelea kufanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na CAG ili kuokoa hasara itokanayo na ujenzi wa soko hilo.


Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.