• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo

Halmashauri zaagizwa kuitumia vizuri mifumo ya kielektroniki

Imewekwa tar.: June 11th, 2018

Na Mathew Kwembe, Kagera

Watendaji wa Halmashauri nchini wameagizwa kuitumia vizuri mifumo mbalimbali ya kielektroniki iliyowekwa na Serikali kwa kushirikiana na Mradi wa PS3 katika halmashauri zote 185 nchini ili mifumo hiyo iweze kufanya kazi yake kwa malengo yaliyokusudiwa.

Agizo hilo limetolewa leo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Kamishna wa Polisi Diwani Athuman wakati akifungua mafunzo ya siku nne ya Mfumo wa Epicor toleo la 10.2 kwa Waweka hazina, Wahasibu na Maafisa Wasimamizi wa Fedha kutoka Mikoa ya Mara na Kigoma yaliyofanyika mjini Bukoba.

Alisema kuwa mifumo hii imetumia fedha nyingi kuisimika na hivyo watendaji wa halmashauri hawana budi kulijua hilo na kuhakikisha kuwa wanaitumia katika kuboresha utendaji wao wa kazi na pia kuiwezesha serikali kutekeleza majukumu yake ya kuwahudumia wananchi.

Katibu Tawala huyo alisema kuwa ipo mifano kwa baadhi ya halmashauri katika mkoa wake ambazo watendaji wake wamekuwa wakishindwa kutekeleza majukumu yao vizuri.

Alisema kuwa halmashauri nyingi nchini zimewekewa mfumo wa ukusanyaji mapato lakini mifumo hii haitumiki kwa kiwango kilichokusudiwa.

Alisema halmashauri zimenunua vifaa vya kukusanyia mapato (POS) kwa ajili ya kuboresha ukusanyaji na kudhibiti udanganyifu na hila wakati ukusanyaji mapato lakini baadhi ya halmashauri zimeweka vifaa hivyo stoo.

Pia alisema kuwa uchunguzi walioufanya katika baadhi ya halmashauri za mkoa wake wamebaini kuwa baadhi ya watendaji wa halmashauri wasio waaminifu wamekuwa wakikusanya mapato kwa kutumia vifaa hivyo vya kielektroniki lakini fedha zinaishia mifukoni kwa watendaji hao.

“Mfano hapa Kagera tuna halmashauri ambazo pamoja na kuwekewa mifumo hii ya ukusanyaji mapato zimeshindwa kuitumia mifumo hiyo kukusanya mapato vizuri,” alieleza.

Akitolea mfano wa halmashauri ya wilaya ya Karagwe, Kamishna Athumani alisema kuwa uongozi wa mkoa wa Kagera umelazimika kutuma wataalamu kutoka taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa kwenda katika halmashauri hiyo ili kufanya uchunguzi wa uhakiki wa mifumo yao ya ukusanyaji mapato.

Hivyo Katibu Tawala huyo aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kutoka Mara na Kigoma kuhakikisha kuwa wanayatumia vizuri mafunzo hayo kwenda kuboresha utendaji wao wa kazi.

Aidha Kamishna Diwani aliwataka Wakurugenzi wa halmashauri nchini kuhakikisha kuwa wanatekeleza wajibu wao vizuri.

Alisema kuwa watendaji wa halmashauri hawana budi kujitafakari kama wanazitendea haki taaluma zao pale wanapotekeza majukumu yao kwani ni wajibu wao kuhakikisha kuwa wanatenda haki kwa umma kwa kutekeleza vizuri majukumu waliyopewa.

Kwa upande wake Meneja wa Mradi wa PS3 mkoa wa Kigoma Bwana Simon Mabagala alieleza kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo watendaji hao kutambua maboresho yaliyofanywa na serikali ya kuwa na mfumo mmoja wa usimamizi wa fedha za umma.

Mwakilishi wa washiriki wa mafunzo Bibi Mercy Swai ambaye ni Mwekahazina wa halmashauri ya Wilaya ya Kakonko kutoka mkoani Kigoma alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwao kwani yatawawezesha kumudu kuutumia mfumo wa Epicor ulioboreshwa.

Aliongeza kuwa matoleo yaliyopita yalikuwa na changamoto mbalimbali lakini mfumo wa Epicor toleo la 10.2 utawawezesha kuondokana na changamoto zilikuwepo katika mifumo iliyopita ya Epicor.



Matangazo

  • MAJINA YA WALIOPATA AJIRA KADA ZA AFYA NA UALIMU June 26, 2022
  • ORODHA YA WAKUU WA KITENGO CHA FEDHA YENYE MABADILIKO 5-5-2022 May 06, 2022
  • Kazi za muda za makarani na wasimamizi wa Sensa 2022 May 05, 2022
  • MUDA WA NYONGEZA MAOMBI YA AJIRA ZA TAMISEMI 2022 May 04, 2022
  • Taarifa ya Kitengo Manunuzi na Ugavi, April 2022 April 04, 2022
  • Safeguard Documents for TACTIC Project March 30, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • BASHUNGWA AWAAGIZA VIONGOZI WA MIKOA NA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA KUTANGAZA MIRADI YA MAENDELEO.

    July 02, 2022
  • Mameya, Wenyeviti wa Halmashuri watoa kongole kwa Rais Samia kuibadili Dodoma

    June 30, 2022
  • MAMEYA, WENYEVITI WA HALMASHAURI SIMAMIENI UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO- PROF. SHEMDOE

    June 30, 2022
  • WAZIRI MKUU MAJALIWA AWAFUNDA MAMEYA, WENYEVITI WA HALMASHAURI

    June 27, 2022
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.