• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

DMDP Waipongeza Serikali, Usimamizi mzuri wa Miradi

Imewekwa tar.: May 22nd, 2019

Mtaalam wa Mipangomiji na msimamizi wa mradi wa DMDP Erick Dickson, amepongeza mwenendo wa utekelezaji wa mradi wa uendelezaji Jiji la Dar es Salaam (DMDP) unaosimamiwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OR-TAMISEMI).

Erick ametoa pongezi hizo tarehe 20 Mei, 2019 mara baada yakurejea nchini, wakati wa mkutano mkuu wa tathimini ya mwaka ya Miradi ya  DMDP,  Mradi wa Uimarishaji Halmashauri za Miji (ULGSP) na Mradi wa Uimarishaji Halmashauri za Miji ya Kimkakati (TSCP) unaofanyika kwa siku tano Jijini Dar es Salaam .

“Mtazamo wangu na wa timu ya Benki ya Dunia ni kuwa DMDP ipo kwenye mwelekeo sahihi na kazi nyingi zinaendelea kutekelezwa vizuri. Pongezi nyingi ziende kwa timu nzima inayosimamia mradi wa DMDP na wote wanaofanya kazi bila kuchoka kuhakikisha kuwa DMDP inaleta mafanikio na mabadiliko makubwa. Huu Ndiyo ujumbe tutakao anza nao katika mkutano huu,” alisema Erick.

Ndugu Erick alieleza kuwa, mradi unatekelezwa katika mazingira ambayo kazi nyingi zinafanyika kwa pamoja ikiwepo, Kupandisha hadhi makazi yaliyopangwa kiholela, ujenzi wa barabara zinazounganisha barabara za mwendokasi na barabara kuu (feeder roads), barabara za Mitaa pamoja na mifereji ya maji ya mvua, masoko, vituo vya daladala na nyinginezo.

“ Pamoja na hayo yote taarifa ninazopata ni kwamba tuna mradi ambao tunafanya vizuri na kuleta mabadilliko makubwa pamoja na kuwepo kwa changamoto za kawaida hili ni  jambo la kujivunia,” alisisitiza.

Naye Mratibu wa Kikundi kazi cha utekelezaji wa miradi inayofadhiliwa na Benki ya Dunia (WBWG) Mhandisi, Davis Shemangale alisema kwamba, mradi wa DMDP unatekelezwa ukienda sambamba na Mpango Makakati wa Taifa wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini ifikapo 2025.

“kwa kuzingatia kuwa Dar es Salaam inachangia sehemu kubwa ya pato la Taifa, DMDP hadi sasa imewezesha kwa kiasi kikubwa kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji na kuongeza mawasiliano na muunganiko wa bararabara kwa maeneo ambayo yalikuwa ni vigumu kufikika hapo awali, hali hiyo imeongeza uimarikaji wa shughuli za kiuchumi” alisema Shemangale.

Mhandisi Shemangale alisema, madhumuni ya Mkutano huo ni kufanya mapitio na kutoa tathmini ya mradi ulipofikia katika utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu, maswala ya matumizi ya fedha na utekelezaji wa maswala ya kimazingira na usalama kama yanatimiza vigezo vya kimataifa vilivyoainishwa. Shemanagale  alieleza kuwa, mradi wa DMDP hadi kufikia takribani ni nusu ya utekelezaji wake tayari umekukumbana na changamoto mbalimbali, ukiwapo msongamano mkubwa uliopo katika Jiji ambapo ni takribani ni asilimia 80 ya makaazi yamejengwa kiholela.

“Jiji ni kubwa na linamsongamano Mkubwa na changamoto mojawapo ni upatikanaji wa malighafi za ujenzi katika naeneo ya mbali na mji. Pia ulipaji fidia umekuwa na changamoto mbalimbali zilizosababisha utekelezaji wa mradi kuchelewa katika baadhi ya maeneo,” alisema Mhandisi Shemangale.

Katika hatua nyingine aliishukuru Benki ya Dunia na hasa kiongozi wa timu ya Mradi Erick Dickson kwa kushirikiana kikamilifu na Serikali na kufanya kazi bila kuchoka, ili kuhakikisha changamoto zote za mradi zinashughulikiwa ili kuhakikisha mradi unatekelezwa na kukamilika katika ubora uliokusudiwa.

Mradi wa DMDP unatekelezwa katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa gharama ya shilingi bilioni 660, ambazo ni mkopo nafuu kutoka Benki ya Dunia, huku serikali ikichangia shilingi bilioni 25 kama sehemu ya mchango wa serikali.

Anaandika Rapahael Kilapilo- TAMISEMI-DSM.

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.