• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Dkt. Chaula : Kituo cha afya cha Nzera kimejengwa kwa viwango

Imewekwa tar.: September 1st, 2018

Naibu Katibu  Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia afya Dkt. Zainabu Chaula  ameipongeza Halmashauri  ya  Wilaya ya Geita  kwa kusimamia kwa weledi ujenzi wa kituo cha Afya Nzera kilichopo Mkoani Geita ambacho kwa sasa kinatoa huduma kwa jamii.

Akiwa kwenye ziara ya Kikazi Mkoani Geita Dkt. Zainabu Chaula amesema kuwa ameridhishwa na ukarabati pamoja na ujenzi wa kituo hicho kwa kujengwa kwa kuzingatia viwango vya hali ya juu  kwa gharama ya shilingi milioni 500 zilizotolewa na Serikali.

“Nimeridhishwa na ujenzi wa Kituo cha Afya cha Nzera ambapo mpaka sasa kimeweza kujenga majengo saba ya kutolea huduma ya afya ikiwemo duka la dawa, Chumba cha kuifadhia maiti, wodi ya wazazi, chumba cha upasuaji, maabara na nyumba nne za watumishi” Anafafanua Dkt.Chaula

Dkt. Chaula amesema kuwa kufanya kazi kwa pamoja ndipo kulipofikisha hapo walipo na kuwezesha kituo hicho kukamilika kwa wakati na kuweza kuanza kutumia majengo hayo kwa ajili ya kutolea huduma za afya kwa jamii ya Halmashauri hiyo

Anaendelea kufafanua kuwa baada ya kufanya utafiti wa kina na  kugundua kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ina wakazi  7036 lakini katika wakazi hao  kulikuwa na vituo 5 vya afya  vilivyokuwa vikitoa huduma na vituo hivyo havikuwa vikitoa huduma stahiki za afya ndipo Serikali ilipoamua kuwekeza fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya afya katika kituo hicho.

Aidha amewapongeza wananchi kwa mchango mkubwa wa kuhakikisha kituo kinakamilika kwa wakati na kutumia nguvukazi katika ujenzi wa kituo hicho hivyo amewasisiriza kufanyakazi kwa umoja, mshikamano na  moyo wakujitolea ili kuunga mkono juhudi za  Serikali katika jitiada zake za kuleta maendeleo kwa jamii

Wakati huohuo mbunge wa Jimbo la Geita  Mhe.Joseph Kasheku Msukuma  ameipongeza Serikali kwa kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha afya cha Nzera jambo ambalo limesaidia wananchi wa jimbo hilo kupata huduma za afya katika eneo la karibu wanapoishi tofauti na awali walikuwa  wanatembea muda mrefu kufuata huduma hiyo.

Amesema kuwa  kata zinazopata huduma za afya katika kituo hicho ni Kata ya Kubasa iliyoko umbali wa  kilometa 90  na Nkombe iliyoko  umbali wa kilometa 40, hivyo amemuomba Dkt. Zainabu Chaula kuongeza  vituo vya afya  katika maeneo hayo ili kuwapunguzia wananchi shida ya kutafuta huduma ya afya.



Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Waziri Kairuki atoa maagizo DART
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.