• Kituo cha Huduma kwa Wananchi |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
    • Muundo wa Wizara
    • Idara na Vitengo
    • Taasisi za Wizara
    • Majukumu ya Idara na Vitengo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Taasisi
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Umma
    • Youtube Channel
    • Instagram
    • Twitter
    • Facebook
  • Machapisho
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
    • Green and Smart Cities
    • Miongozo ya Kilimo
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Michoro ya Ujenzi
    • Msimbazi Basin Development Project
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App
    • Nyaraka Mbalimbali
  • Mifumo
    • Mikopo ya 10% ya Halmashauri
    • Ajira za Elimu & Afya
    • Mfumo wa Tarifa za Shule (SIS)

Mwanza, Songwe kucheza nusu fainali kesho UMISSETA Soka wavulana

Imewekwa tar.: June 18th, 2019

Na Mathew Kwembe, Mtwara

Michuano ya UMISSETA inayoendelea mjini Mtwara imefikia hatua ya nusu fainali kwa upande wa soka wavulana ambapo katika michezo iliyomalizika leo jioni, timu za soka wavulana kutoka mikoa ya Lindi, Ruvuma, Mwanza na Songwe zimefanikiwa kuingia hatua ya nusu fainali baada ya kuwalaza wapinzani wao akiwemo bingwa mtetezi Tanga ambayo ilitolewa na Lindi.

Kwa matokeo hayo timu ya soka wavulana kutoka mkoa wa Lindi itakutana na Ruvuma kwenye nusu fainali ya kwanza inayotarajiwa kucheza kesho saa nane mchana na kufuatiwa na nusu fainali ya pili itakayowakutanisha vigogo Mwanza watakaochuana na timu ngumu ya Songwe.

Timu ya kwanza kuingia hatua ya nusu fainali ilikuwa ni timu machachari ya kutoka  mkoa wa Lindi ambayo iliitoa timu ya mkoa wa Tanga kwa penati 3 kwa 1 baada ya kutoka suluhu ya bila kufungana baada ya dakika tisini za mchezo.

Pambano lingine la robo fainali lilizihusisha timu za kutoka mikoa Ruvuma na Kilimanjaro ambapo timu ya soka ya mkoa wa Ruvuma ambayo inaundwa na wachezaji 8 kutoka kwenye kituo cha michezo cha shule ya sekondari Ruhuwiko iliyopo nje kidogo ya Manispaa ya songea iliwafunga timu ya Kilimanjaro kwa magoli mawili kwa bila.

Katika mechi zilizomalizika jioni hii timu za Songwe na Manyara na Mbeya na Mwanza zilimenyana vikali katika michezo mingine ya robo fainali ambapo Songwe waliwalaza Manyara kwa goli moja kwa sifuri na Mwanza waliifunga Mbeya kwa magoli ya penati 5 kwa 3 ya Mbeya baada ya timu hizo kutoka suluhu ya bila kufungana ndani ya dakika 90 za mchezo.

Hata hivyo Mwanza walikuwa na kila sababu ya kushinda mchezo huo kwani kwenye dakika ya 72 walikosa goli la wazi baada ya penati yao kupanguliwa na golikipa wa Mbeya Gerald Hatson na kuokolewa na mabeki wa timu hiyo.

Mara baada ya mchezo huo, Kocha wa Mwanza Mwalimu Tito Mkami amesema kuwa vijana wake walipambana kufa na kupona lakini akawasifu timu ya Mbeya kwa namna ilivyowasumbua na akakiri kuwa  timu hiyo ngumu kwani iliwapa wakati mgumu wachezaji wake wakati wote wa mchezo.

Aidha Mwalimu Mkami alitoa wito kwa Chama cha soka nchini TFF kutoshirikisha mashindano mengine pindi michuano inayoandaliwa na serikali ya UMISSETA na UMITASHUMTA inapofanyika ili kutosababisha michuano hii kukosa wachezaji muhimu kwa timu zao

Naye nahodha wa timu ya soka ya Mwanza Kimwaga Kalunga ambaye ni Mwanafunzi pekee anayechezea timu hiyo kutoka shule maalum ya soka ya Alliance ambaye alisema kuwa hawaihofii timu ya Songwe bali wanaiheshimu kwani timu zote zilizoingia hatua hiyo ni ngumu.

Mapema kesho asubuhi michezo ya nusu fainali kwa upande wa soka wasichana itachezwa katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara ambapo mchezo wa kwanza utawakutanisha wababe Dar es salaam watakaotoana jasho na timu kutoka mkoa wa Iringa, na mchezo mwingine utawakutanisha miamba Mwanza watakaochuana na Ruvuma.

Kwa upande wa mpira wa mikono matokeo ya robo fainali ya mchezo huo iliyochezwa leo jioni inaonyesha kuwa timu za Geita  na Unguja wavulana zimefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali na zimepangwa kucheza kesho, huku nusu fainali nyingine itawakutanisha Tanga na Morogoro.

Katika mpira wa mikono wasichana, timu zilizofuzu ni Unguja ambao watakuna kesho na Morogoro na Songwe watakaocheza na Mbeya.

Mchezo mwingine ambazo timu zilizofuzu zimejulikana ni netiboli ambapo timu za Morogoro, Tanga, Dar es salaam na Mwanza zimefuzu hatua hiyo ambapo michezo hiyo itachezwa kesho kwa Tanga kukutana na Mwanza na Morogoro kucheza na Dar es salaam.

Katika mchezo wa kikapu kwa upande wa wavulana timu zilizofuzu hatua ya nusu fainali ni Pwani, Unguja, Tanga na Shinyanga ambapo kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa Pwani itacheza na Unguja na Tanga itachuana na Shinyanga.

Kwa upande wa  mpira wa kikapu wasichana Kilimanjaro itamenyana na Mwanza na Morogoro watacheza na jirani zao Dar es salaam.

Matangazo

  • Orodha ya waliopata vibali vya Uhamisho Septemba - Disemba 2022 (OR - TAMISEMI) January 21, 2023
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Kwanza Waliorudia Mtihani January 15, 2023
  • Matumizi ya Lugha ya Kiswahili na Kingereza January 14, 2023
  • Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2023 December 14, 2022
  • Orodha ya Waliopangwa kwenye Vituo vya Kazi Kada za Afya (Awamu ya Pili) Agosti 2022 August 30, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA AJIRA KWA KADA ZA AFYA (Marudio) July 20, 2022
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • LAAC YAPOKEA TAARIFA KUHUSU UTAWALA NA UENDESHAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

    March 14, 2023
  • SERIKALI YAWEKA MIKAKATI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MENDELEO, UKUSANYAJI NA UDHIBITI WA MAPATO KATIKA HALMASHAURI

    March 13, 2023
  • WAUGUZI NA WAKUNGA WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI YA KAZI

    March 13, 2023
  • ACHENI KUTUMIANA NYARAKA ZA SERIKALI KWENYE MITANDAO YA KIJAMII NA BARUA PEPE BINAFSI - DKT. MPANGO

    March 13, 2023
  • Angalia zote

Video

Taarifa ya Ukusanyaji wa Mapato ya Halmashauri, kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2021/22
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Mfumo wa ugavi-Wizara ya Afya
  • Wazo la Waziri
  • Michoro ya Ujenzi
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Ajira za Tamisemi
  • Mfumo wa vibali vya kusafiri nje ya nchi
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania

    Simu: +255 262 321 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.