
Vumbi Latimuka UMITASHUMTA Iringa: Dodoma, Songwe Zatingisha katika Mpira wa Mikono
OR-TAMISEMI
Mashindano ya UMITASHUMTA ngazi ya taifa yameanza kwa kishindo katika viwanja mbalimbali vya michezo vilivyopo mkoani Iringa, huku viwanja vya Chuo cha Ualimu Klerruu, Shule ya Sekondari ya Wasichana Iringa, na Lugalo vikianza kutimua vumbi kufuatia mechi za hatua ya makundi.
Katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Iringa, michezo ya mpira wa mikono kwa upande wa wavulana imepigwa kwa ushindani mkubwa. Timu ya Songwe ilianza kwa kishindo kwa kuichapa Kigoma kwa mabao 15–9, huku Morogoro ikiitandika Shinyanga kwa magoli 16–11.
Mkoa wa Dodoma umeonyesha uwezo mkubwa baada ya kuifunga Kilimanjaro kwa magoli 20–6 kabla ya kuendeleza ubabe kwa kuichapa Singida kwa mabao 18–10 na kujinyakulia pointi muhimu katika kundi lao.
Mashindano haya yanaendelea kuvutia mashabiki wengi huku wachezaji wakionesha vipaji vya hali ya juu katika kuwania nafasi za juu kuelekea hatua ya makundi.
Comments
Please sign in to leave a comment.
Matangazo Muhimu
Soma matangazo na taarifa rasmi ili kuendelea kufahamu shughuli zinazotekelezwa na Wizara.
Tangazo la kuitwa kazini ajira za TMCHIP 2025
Mpango Mkakati wa Usimamizi wa Takwimu wa Ofisi ya Rais TAMISEMI - 2024/25 -2028/29
Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kitongoji 2024
Kanuni za Uchaguzi wa mwaka 2024
Tangazo la Uchaguzi

