• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App

Wakurugenzi zingatieni miongozo ili kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma

Imewekwa tar.: January 30th, 2019

Majid Abdulkarim na Mathew Kwembe

Serikali imewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuzingatia sheria, taratibu na miongozo ya matumizi ya fedha za serikali ili kupunguza matumizi mabaya ya fedha za serikali zinazotolewa kwa ajili ya Elimu.

Akifunga mafunzo elekezi kuhusu utekelezaji wa mradi wa lipa kulingana na matokeo katika Sekta ya Elimu (EP4R) jana jijini Dodoma, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Afya)  Mhe. Josephat Sinkamba Kandege alisema kuwa serikali itahakikisha kuwa hakuna shilingi hata moja itakayopotea wakati wa utekelezaji wa miradi hiyo.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuhakikisha kuwa fedha yote itakayotolewa kwa ajili ya miradi inayopelekwa halmashauri ama iwe imetoka serikalini au kwa wahisani haitumiki kinyume na malengo yaliyokusudiwa

“Kila shilingi tunataka iwe na tija, hivyo nawataka wakurugenzi wa halmashauri na watendaji wengine mhakikishe kuwa mnafuata miongozo ili muepuke hoja za ukaguzi,” alisema

Aliongeza kuwa kila kiongozi  anatakiwa  kufanya kazi kwa weledi  na kuacha tabia ya kufanyakazi kwa mazoea na kuzingatia  miongozo na maelekezo  ya matumizi ya fedha zinazotolewa na Serikali  pamoja na wadau wa maendeleo  ili kuepuka hoja za wakaguzi.

Pia aliwaagiza watendaji hao kusimamia  na  kufatilia utekelezaji wa miradi hasa ujenzi wa miundombinu ya shule ili ikamilike kwa wakati  na kuwashirikisha  kamati, bodi na jamii inayozuguka  katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na  kupunguza ghalama zisizoza msingi, kutoa ajira kwa jamii husika na kuharakisha katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Alisema matumizi ya fedha yanayotumika katika miradi husika yaendane na thamani ya mradi husika ili kuhakikisha sekta ya elimu inapata matokeo chanya.

Aidha Mhe. Kandege alisema ili kuthibiti ubora wa elimu nchini halmashauri  zihakikishe shule zinakaguliwa kwa wakati  muafaka na changamoto zinazobainishwa na wathibiti ubora zifanyiwe kazi haraka ili watoto wa kitanzania wapate elimu bora.

“Wakaguzi wa Halmashauri toeni ushirikiano kwa wathibiti Ubora wa Elimu na Mafunzo elekezi kwa wakuu wa shule juu ya umuhimu wa kutekeleza ukaguzi wa ndani ya shule pale panapo kuwa na changamoto mawasiliano  yafanyike kwa wakati kupitia  Ofisi ya Mkoa ili  muweze kufikia malengo ya pamoja,” alisema.

Mapema kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri kufunga kikao hicho, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa  Elimu kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia Elimu ya Msingi Dkt. George Jidamva alisema changamoto kubwa waliyoiona kwenye utekelezaji wa mradi huo ni kwa baadhi ya watendaji kushindwa kujibu hoja za ukaguzi kwa kukosa vielelezo muhimu kama risiti na orodha ya malipo.

Changamoto nyingine ni kutofautiana kwa ubora wa majengo kati ya halmashauri na halmashauri licha ya kuwa ramani za miundombinu hiyo kufanana na hivyo kukosekana kwa thamani ya ubora kutokana na baadhi ya majengo kujengwa chini ya kiwango.

Mradi lipa kulingana na matokeo katika sekta ya elimu ( EP4R) ulianza Septemba, 2014 kwenye Mamlaka za serikali za mitaa kwa kupokea kiasi cha shilling bilioni 77.98 na kwa sasa halmashauri hizo zinatarajia kupokea kiasi cha shilling biloni 40 kutoka kwa wadau wa maendeleo ambazo zitatumika  kwa mujibu wa maelekezo yatakayo tolewa na mamlaka husika.

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Kafanyeni Tohara kupunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi

    March 04, 2021
  • Uhaba wa Saruji wachelewesha ujenzi wa barabara za Mji wa Serikali

    March 03, 2021
  • Natoa siku siku 12 mtatue kero za soko la Ndugai na Stendi kuu ya Mabasi- Waziri Jafo

    March 03, 2021
  • Agizo la ujenzi wa vyumba vya madarasa 2257 latekelezwa

    March 02, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.