• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App

Tosiri aibuka kinara fainali za mita 200 Umisseta

Imewekwa tar.: June 15th, 2019


Na Mathew Kwembe, Mtwara

Mwanafunzi Ismail Hussein Tosiri kutoka shule ya sekondari Makongo ya jijini Dar es salaam, amefanikiwa kunyakua medali ya dhahabu kwa upande wa wavulana kwenye fainali za mashindano ya Umoja wa Michezo ya Shule za Sekondari (UMISSETA)  iliyofanyika leo katika viwanja vya chuo cha ualimu Mtwara.

Ismail ambaye pia ni bingwa wa riadha kwa nchi za Afrika Mashariki kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 21 aliwaacha kwa mbali wanariadha wenzake Benedict Matias  kutoka Pwani ambaye alishika nafasi ya pili na Amos Charles  pia wa pwani ambaye alishika nafasi ya tatu.

Licha ya kukiri kuwa mashindano ya mwaka huu yalikuwa magumu kwake kutokana na ushindani wa hali ya juu uliojitokeza kwenye mbio hizo, Ismaili alijigamba kuwa siri ya mafanikio yake ni mazoezi makali aliyokuwa anayafanya kabla ya kuanza kwa mashindano hayo.

Amesema kuwa hivi sasa anajipanga vema ili aweze kufanya vizuri kwenye mashindano ya ya shule za Sekondari Afrika Mashariki FEASA yaliyopangwa kufanyika mkoani Arusha mapema mwezi wa nane mwaka huu.

 Kwa upande wa wasichana bingwa wa mbio za mita 200 ni Thereza Bernard kutoka Simiyu ambaye aliwashinda wenzake Emmy Hosea kutoka Singida aliyeshika nafasi ya pili na Hermegrida Manifred kutoka Pwani alishika nafasi ya tatu.

Katika fainali za mita 800, bingwa wa mbio hizo mwaka huu kwa upande wa wavulana ni mwanafunzi Japhet Joseph kutoka Singida ambaye alijinyakulia medali ya dhahabu, nafasi ya pili imeshikwa na Abrahamu Chapa wa Morogoro aliyejinyakulia medali ya fedha na medali ya shaba imekwenda kwa William Mguya kutoka Manyara ambaye alishika nafasi ya tatu.

Katika fainali za mita 800 wasichana, nafasi ya kwanza imechukuliwa na mwanariadha Gaudensia Manero kutoka mkoa wa Pwani, nafasi ya pili imechukuliwa na Rahel Nira wa Simiyu na nafasi ya tatu imekwenda kwa Regina Deogratius wa Pwani.

Kufuatia kukamilika kwa mbio hizo, mjumbe wa kamati ya ufundi wa chama cha riadha Tanzania Robert Kalyahe alisema kuwa wanariadha walioshindana katika mbio za mita 200 na 800 mwaka huu walishindwa kufikia viwango vya mwaka jana na miaka iliyopita kwa vile wengi wa waliokuwa wakishiriki mashindano hayo ni wapya kwa vile wazoefu wengi wamekwishamaliza elimu yao ya sekondari.

Kadhalika amesema kuwa wanafunzi wengi walioshiriki mbio hizo mwaka huu walikimbia bila ya kuwa na viatu jambo ambalo amesema kuwa siyo sawa kwani limewanyika ushindi vijana wengi waliokuwa na vipaji.

“Wanariadha walioshinda wengi wao walikuwa na viatu vya kukimbilia (spikes) ambavyo kariakoo bei yake haizidi shilingi 30,000, ukilinganisha na viatu vinavyotumiwa na wacheza mpira wa miguu ambavyo ni karibu shilingi 90,000, “ amesema Kalyahe, na kuongeza:

“Jamii inapaswa kuwekeza kwenye mchezo wa riadha kama kweli tunataka kurudisha heshima ya mchezo huu kama ilivyokuwa miaka ya nyuma ya ushiriki wa kina Nyambui, na Bayi.”

Kalyahe amesema kama kweli tunataka kushinda kimataifa jukumu la kutafuta vipaji vya wanamichezo wanariadha linapaswa kwenda hadi vijijini badala ya kuishia kwenye akademi za michezo.

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Natoa siku siku 12 mtatue kero za soko la Ndugai na Stendi kuu ya Mabasi- Waziri Jafo

    March 03, 2021
  • Agizo la ujenzi wa vyumba vya madarasa 2257 latekelezwa

    March 02, 2021
  • Waziri Jafo ataka Shilingi Bilioni 245 za Miradi ya Maendeleo zitumike kwa wakati

    March 01, 2021
  • Serikali yalegeza masharti mikopo ya asilimia 10

    February 27, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.