• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

“Timu za Afya Mikoani Mjipange Vizuri” Dkt. Gwajima

Imewekwa tar.: February 8th, 2019

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa, anayeshughulikia afya, Dkt. Dorothy Gwajima, ameziagiza timu za Afya za Mikoa (Regional Health Management Team- RHMT) yote nchini, kujitathmini hali yao ya utendajikazi na kuona kama wanatija inayokubalika kwa taifa.

Gwajima ameitoa kauli hiyo, alipokuwa akizungumza na timu ya Afya ya Mkoa wa Dodoma inayo ongozwa na James Kiologwe, Mganga Mkuu wa Mkoa huo wakati alipofanya ziara yake ya kwanza toka ateuliwe kushika wadhifa huo Januari 08,2019 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.

Akiwa katika ziara hiyo, Gwajima alisema kila mmoja katika timu hiyo inayo simamia afya wajifanyie tathmini dhidi ya utendaji wao huku akisema, ametumia jukwaa hilo la timu ya Dodoma lakini na waliopo katika Mikoa Mingine yote nchini nao wajitathmini huko huko walipo wasingojee ziara yake ndio waanze kubadilika.

“Tatizo kubwa tulilonalo ni uratibu wa kazi, jukumu moja unakuta linakuwa na uratibu usiofahamika jambo ambayo wakati mwingine hata mtekelezaji anashindwa afanye lipi na aache lipi alisema Gwajima, na kuongeza kuwa, hili ndilo nililo ligundua ndani ya siku zangu 30 za kuwepo katika ofisini yangu mpya”.

Timu za Afya za Mkoa zimetakiwa kutambua kwamba, majukumu yao ndio maduka yao wanaotakiwa kuyafanyia kazi usiku na mchana huku wakionesha matokeo chanya ya kile wanancho kifanya kwa kutoa taarifa kwenye ngazi husika.

Gwajima amesisitiza kwamba katika dira aliyonayo kwenye kutekeleza majukumu yake mapya ni pamoja na kuzingatia, uratibu (Cordination), matokeo chanya (Result/Productivity), huduma bora (Good Services) kwa mteja pamoja na kuwajali wateja (Customer care), hivyo akawataka wajumbe wa timu zote za afya za mikoa Tanzania Bara, kulijua hilo na kulizingatia.

“Inatia hofu sana, unakuta mtu ni mratibu wa kitengo fulani katika ngazi ya Mkoa, lakini hata siku moja hajafanya ziara wilayani kwenda kujionea changamoto zilizopo na kushauri nini chakufanya, mimi niwaambie wakati nikiwa Mganga Mkuu wa Wilaya kuna mambo tulikuwa tunaibua katika ngazi ya wilaya na badae yanakuwa na maamuzi kwenye ngazi ya taifa” alisema Gwajima.

Gwajima akawataka wajumbe wote wa timu za mikoa kufanya kazi kiteknolojia ili kuongeza tija ya utendaji kazi wao lakini pia matumizi ya teknolojia iwe ni chachu ya wao kufanya kazi na kuonesha matokeo (Productivity).

“Serikali imeajiri watumishi Elfu sita (6,000) wa afya, je mmesha jiuliza katika kufanikisha utendaji wenye tija mmewatumiaje hususan katika matumizi ya teknolojia?” alihoji Gwajima, na kusema, lazima tuhakikishe wanajua namna yakuwafikia wananchi hata kwa njia ya mtandao na kutoa ushauri ili kupunguza misongamano katika vituo vyetu vya kutolea huduma, kwani sio kila mgonjwa aende hospitali wengine wanahitaji ushauri tu.” Alisisitiza Gwajima.  

Awali akiwa katika  kikao na Wajumbe wa Sekretarieti ya Mkoa, Katibu Tawala wa Mkoa huo Maduka Kessy, alimuelezea Naibu Katibu Mkuu kwamba, ushirikishwaji wa maamuzi yaliyo mengi yamekuwa yakifanywa na Wizara moja kwa moja na kukosa uratibu wa Mkoa hali ilizua mkanganyiko wa maamuzi, sambamba na  kuwakilisha kilio chake cha uhaba wa Magari ya viongozi katika mkoa huo wakiwapo waheshimiwa Wakuu wa Wilaya.

Dkt. Dorothy Gwajima aliteuliwa kushika wadhfa huo wa Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya OR-TAMISEMI, akichukua nafasi iliyo achwa wazi na Dkt. Zainab Chaula aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya nah ii ni ziara yake ya kwanza kufanya katika Sekretarieti ya Mkoa.

Anaandika: Atley Kuni


Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato

    January 21, 2021
  • Dodoma wapongezwa, wapewa miezi 5 kukamilisha ujenzi wa barabara

    January 20, 2021
  • Shule ya Msingi Nkuhungu yapewa siku 14 kukarabatiwa

    January 20, 2021
  • Asilimia 10 inavyoibua Wajasiriamali Arusha

    January 19, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.