• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu

TAMISEMI yapokea magari mawili kuboresha afya Mtwara na Lindi

Imewekwa tar.: October 9th, 2018

Na Mathew Kwembe, Dar es salaam

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo amepokea magari mawili yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 200 na kusema kuwa magari hayo yataongeza thamani katika juhudi za serikali za kuimarisha utoaji wa huduma bora za afya katika mikoa ya Lindi na Mtwara.

Kabla ya kuyapokea magari hayo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID) David Thompson katika hafla fupi iliyofanyika katika Ofisi ndogo za TAMISEMI zilizopo jijini Dar es salaam, Waziri Jafo alisema kuwa anatambua kazi nzuri inayofanywa na Serikali ya Marekani kupitia Mradi wa USAID Boresha Afya kanda ya kusini.

Alisema kuwa kwa kutambua kazi nzuri inayofanywa na mradi wa Boresha Afya katika mikoa ya Morogoro, Iringa, Njombe, Lindi, Mtwara na Ruvuma anayo furaha kubwa kushiriki katika hafla hiyo ya kupokea magari hayo yenye thamani ya Tsh.219, 372,136.

“Kwa niaba ya Serikali ya Tanzania ningependa kuwafikishia shukrani zetu za dhat kwa Serikali ya Marekani na wote walio katika mradi huu wa USAID Boresha Afya Kanda ya kusini,” alisema.

Waziri Jafo aliongeza kuwa serikali inajivunia kushirikiana na washirika ambao kweli wanajali hali za raia wa Tanzania.

Alisema kuwa kupitia msaada huo USAID Boresha Afya Kanda ya kusini imeonyesha kweli iko pamoja na watanzania katika kusimamia changamoto za afya nchini.

Waziri Jafo alitoa wito kwa Wakuu wa Mikoa ya Lindi na Mtwara kuhakikisha kuwa magari hayo yanatunzwa kwani hiyo itawatia moyo washirika wa maendeleo kuendelea kutoa misaada zaidi.

Aidha Waziri Jafo alisema Serikali katika kuboresha huduma za afya nchini katika kipindi cha miezi 12 iliyopita imefanikiwa kukamilisha vituo vya afya 210 na hivyo inasubiri kupatiwa madawa kutoka bohari kuu ya madawa nchini.

Aliongeza kuwa katika kipindi cha miezi 18 ijayo Serikali inatarajia kukamilisha ujenzi wa vituo vya afya 340 ambapo vituo 100 vitaweza kutoa huduma ya upasuaji.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt.Zainab Chaula aliishukuru Serikali ya Marekani kwa msaada huo wa magari na kuongeza kuwa msaada huo utajazia juhudi za serikali katika kuboresha huduma za Afya nchini.

Alisema kuwa magari hayo yatatumiwa na Timu ya Usimamizi wa Afya katika Mikoa ya Lindi na Mtwara katika kusaidia na kuimarisha usimamizi wa shughuli zinazohusiana na VVU, uzazi wa mpango, Kifua Kikuu, Malaria, lishe, jinsia, Jamii na nyinginezo zinazohusiana na afya.

Akiongea katika hafla ya makabidhiano hayo, Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa USAID Tanzania David Thompson aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa dhamira yake ya kuboresha viwango vya afya kwa watanzania wote.

“Kupitia msaada huu, Serikali ya Marekani inaungana na Serikali ya Tanzania kurahisisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa watu wote, katika jamii za watu wa Lindi na Mtwara, mkazo zaidi ukiwa kwa wanawake na vijana,” alisema.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mtwara DKT Wedson Sichalwe na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi DKt Genchwele Makenge waliishukuru serikali ya Marekani kwa msaada huo kwani unakwenda sambamba na malengo ya serikali ya kuboresha huduma za afya kwa jamii.

Mradi wa USAID Boresha Afya Kanda ya Kusini ni mradi wa miaka mitano ulioanza oktoba 2016 na unatarajia kukamilisha shughuli zake ifikapo mwezi septemba mwaka 2021 unaotekelezwa na halmashauri 43 kwenye mikoa ya Iringa, Njombe, Morogoro, Lindi, Mtwara na Ruvuma kwa kushirikiana na mashirika ya kitaalamu ya FHI na EngenderHealth na Management and Development for Health (MDH)



Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Serikali yalegeza masharti mikopo ya asilimia 10

    February 27, 2021
  • Vikundi 23 Wilayani Busega vimenufaika na mikopo ya asilimia 10

    February 26, 2021
  • Vikundi 366 Wilayani Kilwa vyanufaika na mikopo ya sh bilioni 1.1

    February 26, 2021
  • Waziri Jafo ataka Zimamoto, Skauti wakomeshe majanga ya moto shuleni

    February 26, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.