• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Serikali yawataka Maafisa Elimu kuleta mageuzi

Imewekwa tar.: September 17th, 2018

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe amesema pamoja na juhudi ambazo serikali inafanya, sekta ya elimu imeshindwa kuleta mageuzi ambayo serikali na wananchi wanayategemea.

Mhandisi Iyombe aliyasema hayo jana  kwenye kikao kazi maalumu kwa watendaji wa elimu katika ngazi ya taifa, mikoa na halmashauri kinachofanyika kwa siku mbili jijini Dodoma.

 “Mwaka 2015 watanzania walipiga kura kwa kutaka mabadiliko, mpaka sasa sekta ya elimu hakuna mabadiliko yaliyofikiwa tofauti na sekta ya afya, bado akili zenu zimelala pale pale,” alisema.

Aliongeza: “Watumishi wasiotaka mabadiliko waondoke wenyewe na kama hawataki kuondoka tutawaondoa hatuwezi kulazimisha mtu kufanya kazi kimazoea na ndiyo maana wengine wanataka kuhonga ili wapate nafasi badala ya kufanya kazi sawasawa.”

Alisema anachukuziwa na kuona mambo hayaendi vizuri kwenye sekta ya elimu wakati maofisa wa elimu ngazi ya mikoa, wilaya na kata wapo na kuonya kuwa endapo kuna kiongozi anaona haweza kuwa chachu wa mabadiliko katika eneo lake basi kiongozi huyo hatoshi.

“ Kuna mambo mengi mabaya yanatokea katika sekta ya elimu lakini viongozi nyinyi mpo tu na hakuna hatua yeyote mnayochukua huku mkisubiri maamuzi kutoka makao makuu.”
Mhandisi Iyombe alitolea mfano tukio la kuchapwa viboko hadi kufa kwa kwa mwanafunzi wa shule ya msingi Kibeta katika Manispaa ya Bukoba ambapo taarifa hiyo aliipata kutoka kwa mdhibiti wa ubora wa elimu wakati maafisa elimu mkoa, wilaya, kata wapo.

“Hakuna tukio baya na la kinyama kama lililofanywa na mwalimu wa shule ya Msingi Kibeta wilayani Bukoba lakini hakuna ripoti zozote zilizotolewa na wahusika na badala yake taarifa ilitolewa na Ofisa Uhakiki Ubora, wakati mwalimu mkuu yupo, afisa elimu kata, wilaya na mkoa wapo na unapowauliza wanasema eti ni tukio kubwa litaonekana kwenye vyombo vya habari yaani Mimi katibu mkuu nifanye kazi na kupeleka taarifa kwa Mheshimiwa Rais kupitia vyombo vya habari wakati uongozi upo kweli nyie mnatosha?” alihoji Mhandisi Iyombe

 Alisema kutowajibika ipasavyo kwa viongozi hao kumechangia hata tabia ya uvujaji na uwizi wa mitihani unaofanywa na baadhi ya shule kwa lengo la kujipatia umaarufu, lakini hakuna hatua zozote zinazochukuliwa.

Aidha, Katibu Mkuu amewataka viongozi hao ambao kwa nyadhifa zao wanaingia kwenye vikao vya maamuzi kuhakikisha wanajenga hoja za nguvu ili halmashauri zitenge fedha kwa ajili ya miundombinu ya shule katika eneo husika.

“ Mnapata nafasi ya kuingia kwenye vikao vya halmashauri, msiende huko kusinzia, mwende mkajenge hoja ili halmashauri zitenge fedha za ndani kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya shule maana wewe ndio unajua hali ya shule zako,” alisema.

Aliongeza: “ Kataeni kuwa na shule za nyasi, watoto wanakaa chini wakati kuna fedha za ndani za halmashauri zipo na kuna maeneo halmashauri zina mapato mengi ya ndani.”

Anaandika Mathew Kwembe- OR TAMISEMI


Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Vikundi 13 Wilayani Kibaha vyanufaika na mikopo ya sh milioni 46

    February 25, 2021
  • Magufuli: Viongozi tatueni kero za wananchi kwa wakati

    February 25, 2021
  • Shilingi Bilioni 3 zakwamua Wanawake, Vijana na Walemavu Geita

    February 25, 2021
  • Vikundi 47 Kondoa vyapewa mikopo ya shilingi milioni 147

    February 24, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.