• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Serikali yapongeza juhudi za usafi wa mazingira kwenye shule za Mkoa wa Manyara

Imewekwa tar.: June 20th, 2020

Serikali imepongeza juhudi za usafi wa mazingira katika shule za mkoa wa Manyara chini ya usimamizi wa uongozi wa Mkoa huo kwenye kutekeleza ajenda ya usafi mazingira katika Shule na kwenye Jamii.

Juhudi hizo zimeshuhudiwa na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais TAMISEMI, anayeshughulikia afya, Daktari Dorothy Gwajima alipofanya ziara katika Mkoa huo akiwa na wataalam wa Ofisi hiyo kwa lengo la kujionea hali ya utekelezaji wa elimu ya afya na mazingira katika shule zinazomilikiwa na Serikali pamoja na taasisi Binafsi.

Akiwa katika shule ya kutwa ya Babati Sekondari, aliusifu uongozi wa Shule kwa kuzingatia kanuni za afya mashuleni kwa jinsi walivyoweza kuwapanga kwa nafasi wanafunzi katika Mabweni wakiwa wameacha nafasi ya kutosha kutoka kitanda kimoja na kingine pia usafi wa vyoo ukiwa wa viwango na pia wakiwa wamezingatia uwekaji wa vyombo vya maji tiririka na sabuni kila eneo la shule.

“Nimekagua hatua kwa hatua kuona jinsi gani mnatekeleza miongozo iliyotolewa na Wizara ya Afya juu ya suala la Afya Mazingira na kwa kweli sina budi kusema mmenikosha sana na hali usafi, yaani chooni ni kusafi kiasi hata huwezi kusikia harufu yoyote, mimi niwatie moyo, endeleeni na usafi huu”, alisema Dkt. Gwajima.

Akiwa katika Shule hiyo ya Babati Day, yeye pamoja na mtaalamu wa lishe kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, walikula chakula kilichokuwa kimeandaliwa kwa ajili ya Wanafunzi kwa lengo la kujionea ubora wa chakula kinachotumiwa na wanafunzi hao.

“Wali huu ni mtamu sana, hivi haya maharage mmenunua wapi”, alisikia Naibu Katibu Mkuu, huku akipeleka Kongole kwa mpishi wa shule hiyo kwa kuwajali wanafunzi na kuwataka kujizatiti katika suala la mboga za majani kwa kuhakikisha Uongozi wa Shule unaratibu kulima mboga mboga kwani wana maeneo mazuri yanayoweza kustawisha mboga za majani kwa wingi.

Akiwa katika Shule ya Sekondari Singe na Hayatul Islamiya, ambazo zote zinamilikiwa na taasisi za dini, Naibu Katibu Mkuu hakusita kuonesha furaha yake kwa namna taasisi hizo zilivyoweza kutekeleza kwa vitendo maelekezo ya Serikali hususan kwenye kipindi hiki cha mlipuko wa ugonjwa wa Corona, ambapo aliweza kujionea Miongozo ikiwa imebandikwa katika shule hizo, lakini pia wanafunzi wakiwa wamechukuwa tahadhari zote za kujilinda dhidi ya maradhi ya ugonjwa huo.

Kwa upande wao uongozi wa shule hizo kwa Nyakati tofauti, waliihakikishia Serikali kuendeleza ushirikiano wao wa karibu katika kutekeleza maagizo yote na miongozo inayotolewa na Serikali katika kutekeleza wajibu wao.

“Ndugu Naibu Katibu Mkuu, naomba nikuhakikishie kuwa, sisi kama shule za taasisi za dini, tutaendelea kushirikiana na Serikali bega kwa bega na kufuata maagizo yote yanayotolewa kwa mustakabali mzuri na thabiti wa afya za Wanafunzi wetu na na ufanisi wa Serikali yetu. Alisema Mkuu wa Shule hiyo Padre Joseph Sakilu.

Naye Mkuu wa Shule ya Hayatul Islamiya Hussen Mwinami alisema, kama shule tayari walishawapokea wanafunzi wote wa kidato cha sita watakaoanza mitihani yao mwishoni mwa mwezi Juni, 2020, lakini pia wamesha weka mazingira rafiki na salama kwa ajili ya kuwapokea wanafunzi watakaoanza masomo yao tarehe 29 Juni, 2020.

Akiongea wakati wa ziara hiyo Afisa Elimu wa Mkoa huo, Bw. Samson Hango, alimuahidi Naibu Katibu Mkuu kuendelea kushirikiana katika utendaji kazi na wataalam wa Afya na taasisi zote zenye mapenzi mem ana suala la usafi wakati wote ili kuhakikisha mkoa huo unaendelea kuwa kinara kwenye suala la usafi wa mazingira katika nyanja zote huku wakiahidi kufuatilia na kuhakikisha kasoro ndogo ndogo zote zilizobainika wakati wa ziara zinatatuliwa mara moja.

Ujumbe huo kutoka Ofisi ya Rais–TAMISEMI, ukiongozwa na Naibu Katibu Mkuu, ulifanya ziara ya kutembelea na kukagua Shule za Sekondari zilizopokea wanafunzi wa kidato cha sita wanaotarajiwa kuanza mitihani yao ya kuhitimu kuanzia Juni, 29, 2020. Katika ziara hiyo Shule na Vituo vya afya vilivyofikiwa na ziara hiyo ni pamoja na Aldergate Sekondari, Babati Day Sekondari na Kituo cha Afya Mutuka, maeneo mengine ni Singe Sekondari, Bonga Sekondari pamoja na Hayatul Islamiya Sekondari.

Na Atley Kuni- MANYARA.

.

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Bil 16.4/- zarejesha hadhi ya Shule za Sekondari za Ufundi nchini

    January 22, 2021
  • Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato

    January 21, 2021
  • Dodoma wapongezwa, wapewa miezi 5 kukamilisha ujenzi wa barabara

    January 20, 2021
  • Shule ya Msingi Nkuhungu yapewa siku 14 kukarabatiwa

    January 20, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.