• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu

Serikali yahimiza upatikanaji wa chakula cha mchana kwa wanafunzi shuleni

Imewekwa tar.: August 19th, 2020

Na. Majid Abdulkarim, Chemba

Serikali imewataka wazazi nchini kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano za kuboresha maendeleo ya elimu kwa kuchangia upatikanaji wa chakula cha mchana shuleni ili kuwajengea wanafunzi mazingira mazuri ya kujisomea na kushindana kimasomo.

Wito huo umetolewa jana na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mamlaka za Mitaa anayeshughulikia Elimu, Mhe. Mwita Waitara wakati wa uzinduzi wa maonyesho ya juma la elimu yanayofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Chemba iliyopo mkoani Dodoma.

Amesema bila wananchi kutia nguvu katika suala la upatikanaji wa chakula cha mchana kwa wanafunzi, lengo la serikali la kuhakikisha kuwa inaboresha elimu kwa kila mtoto halitafikiwa, badala yake kutaibuka matabaka kwa baadhi ya Watoto kupata chakula cha mchana na wengine kukosa kabisa.

Mhe.Waitara ameongeza kuwa wazazi hawana budi kuchangia maendeleo ya Watoto wao kwa kuhakikisha kuwa wanachangia chakula ili Watoto wote wanaosoma katika shule zote za msingi nchini wanapata chakula cha mchana shuleni.

Amesema kwa kufanya hivyo, wazazi watasaidia kupungua kwa changamoto za utoro shuleni, na kujenga mazingira mazuri ya Watoto kusoma ambapo mtoto akipata mlo wa mchana ana nafasi nzuri ya kumsikiliza mwalimu kuliko mtoto aliye na njaa.

Mhe. Waitara amesema kuwa pamoja na juhudi kubwa za Serikali ya awamu ya tano ya Mhe.Rais Dkt John Pombe Magufuli kutoa elimu bure, ikiwa baadhi ya Watoto wataendelea kusoma pasipo kupata chakula cha mchana hakutawajengea mazingira sawa ya kujifunzia.

"Hatuwezi kufanya ushindani ukawa sawa kwa kila mmoja, elimu ni bure sawa lakini kuna watoto wanashinda wakipiga miayo wakati wenzao wamekula, katika hilo unawezaje kuwa na ushindani wa kweli, lazima wengine wawe juu na wengine wabaki chini,"amesisitiza Waitara.

Mhe.Waitara ameeleza kwa kinachofanywa na serikali ni kusaidia watoto wa masikini ambao hawakuwa na uwezo wa kusoma kutokana na kukosa ada hivyo ikaamua kuwekeza huko kwa kutoa fedha jambo lililosaidia ongezeko la uandikishaji watoto wanaoanza shule.

Mapema akimkaribisha Naibu Waziri kuzungumza kwenye maadhimisho hayo, Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Mji wa Kondoa Bi. Annette Nara alieleza kuwa sera ya elimu bila malipo imesaidia kuongeza idadi ya wanafunzi wanaoandikishwa darasa la kwanza na kidato cha kwanza, na kupunguza kiasi kikubwa cha utoro wa wanafunzi shuleni.

Aidha amesema kuwa kutokana na upatikanaji wa chakula shuleni kwa baadhi ya shule zinazotekeleza kupitia Mpango wa kuboresha Elimu Tanzania (EQUIP T) ambapo wazazi wanashirikiana na walimu katika kusimamia mahudhurio ya wanafunzi.

Kabla ya Uzinduzi wa juma la Elimu Mhe. Waitara alipata fursa ya kukagua shule ya Sekondari ya Bihawana ambayo ni mojawapo kati ya shule kongwe 89 zilizopewa fedha kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu.

Pia Naibu waziri alitembelea Shule ya Sekondari ya Wasichana Kondoa na kukagua ukarabati wa jengo la utawala, madarasa, mabweni, vyoo na bafu, Pamoja na miundombinu mingine ya shule hiyo iliyogharimu Shilingi 1,012,729,844.90.

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Serikali yalegeza masharti mikopo ya asilimia 10

    February 27, 2021
  • Vikundi 23 Wilayani Busega vimenufaika na mikopo ya asilimia 10

    February 26, 2021
  • Vikundi 366 Wilayani Kilwa vyanufaika na mikopo ya sh bilioni 1.1

    February 26, 2021
  • Waziri Jafo ataka Zimamoto, Skauti wakomeshe majanga ya moto shuleni

    February 26, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.