• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App

Serikali yagawa Pikipiki 2894 kwa Waratibu Elimu Kata nchini

Imewekwa tar.: July 4th, 2018

Serikali imezindua zoezi la usambazaji wa pikipiki 2,894 kwa Waratibu Elimu kata nchini kwa kutoa wito kwa Maafisa Elimu wa Wilaya kuhakikisha kuwa pikipiki hizo zinawafikia walengwa hao.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa funguo za pikipiki hizo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako, kwa niaba ya Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo, amewataka Maafisa wa Elimu kuhakikisha kuwa pikipiki hizo aina ya Honda zitumiwe na Waratibu Elimu kata.

Alisema kuwa serikali ya Awamu ya tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Magufuli imelipa uzito suala la utoaji wa elimu bora nchini ndiyo maana serikali imeamua kuanzisha mpango wa kutoa elimu bila malipo.

“Ni matumaini yangu baada ya serikali kukubali kutoa pikipiki hizi suala la usimamizi wa elimu katika kata zenu litaenda kufanyika vizuri bila visingizio vyovyote,” alisema.

Mhe.Jafo alisisitiza kuwa  serikali inaenda kuwapatia waratibu wa elimu kata pikipiki hizo na kamwe pikipiki hizo zisitumiwe kwa ajili ya shughuli nyingine zozote mbali na ufuatiliaji na usimamizi wa shule katika kata husika.

“Napenda kulisisitiza jambo hili, pikipiki hizi siyo za kuendea kwenye viti virefu, na pia zisitumike kufanyia shughuli ya bodaboda,” alisema Mhe.Jafo.

Aidha aliwataka Maafisa Elimu Wilaya kuhakikisha kuwa pikipiki hizo aina ya Honda ndiyo zitakazogawiwa kwa waratibu elimu kata na si vinginevyo.

“Sitaki kusikia kuwa waratibu wa elimu kata wamegawiwa pikipiki za aina nyingine badala ya aina hii ya Honda tunazozigawa leo,” alisema.

Alisema serikali inalenga kupandisha ubora wa elimu katika ngazi ya kata, hivyo amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri kuhakikisha kuwa pikipiki hizo zinapatiwa huduma ya mafuta bure katika kipindi cha miezi sita.

Naye Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako alisema kuwa pikipiki hizo zilinunuliwa na Wizara yake kupitia programu ya Lanes ambapo serikali imehakikisha kuwa pikipiki hizo ina vifaa vyote vya usalama barabarani.

Alisema kuwa ni matarajio yake kuwa pikipiki hizo zitawawezesha waratibu elimu kata kuboresha ubora wa elimu katika kata kwa kufanya ufuatiliaji wa mara kwa mara katika shule zao.

Alisema kuwa hatarajii kuona wanafunzi wengi wanaendelea kupata daraja la sifuri, na kamwe shule zisiwe vituo vya kulea watoto badala yake kata ziimarishe usimamizi wa elimu.

Mapema Mwakilishi wa wadau wa Maendeleo Bibi Susan Steven alisema kuwa wao kama wadau wa maendeleo  wamefurahishwa na hatua ya serikali kushirikiana nao katika kuleta maendeleo ya elimu Tanzania.

Anaandika  Mathew Kwembe  OR TAMISEMI

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Uhaba wa Saruji wachelewesha ujenzi wa barabara za Mji wa Serikali

    March 03, 2021
  • Natoa siku siku 12 mtatue kero za soko la Ndugai na Stendi kuu ya Mabasi- Waziri Jafo

    March 03, 2021
  • Agizo la ujenzi wa vyumba vya madarasa 2257 latekelezwa

    March 02, 2021
  • Waziri Jafo ataka Shilingi Bilioni 245 za Miradi ya Maendeleo zitumike kwa wakati

    March 01, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.