• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu

Nzunda ataka walimu kuacha kuwachapa watoto viboko shuleni

Imewekwa tar.: July 25th, 2019

Na Mathew Kwembe, Mwanza

Serikali imewataka walimu kuacha kutegemea matumizi ya viboko shuleni kama njia ya kufundishia kwani inawajengea hofu na uwoga wanafunzi wa kushindwa kujiamini.

Agizo hilo limetolewa leo na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Elimu bwana Tixon Nzunda wakati akizungumza na walimu na wanafunzi wa shule ya msingi ya ufundi ya Bukumbi iliyopo katika wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.

Kwa mujibu wa Naibu Katibu Mkuu, mwenye mamlaka ya kuchapa viboko shuleni ni mwalimu mkuu peke yake, walimu wengine hawapaswi kufanya hivyo labda kwa kibali chake.

Amesema anachukizwa sana na tabia iliyojengeka miongoni mwa baadhi ya walimu ya kudhani kuwa ili aweze kumsaidia mtoto katika elimu yake ni lazima viboko vitumike awapo shuleni.

“Kwenye psychology (saikolojia) mmesoma au kuna authority (mamlaka) inayosema unaingia darasani na fimbo? Wanafunzi wanaenda shambani upo mgongoni mwao na fimbo?” amehoji Naibu Katibu Mkuu na kuongeza:

“Kwa kuwa mmenisomea taarifa yenu ya shule na nimeona matokeo yenu ya darasa la nne na la saba ni mazuri niwasihi hebu acheni kuwachapa watoto,” amesema.

Bwana Nzunda ameongeza kuwa kama hilo watashindwa basi angalau darasani mpige marufuku hakuna mwalimu kuingia na kiboko darasani.

 “Let the children be free ( acheni watoto wawe huru), build confidence ( wajengeeni watoto ujasiri) ili waweze kujiamini, kesho waje kuwa good teachers (walimu wazuri) waipende kazi ya ualimu, wengine wanaichukia kazi ya ualimu kwasababu walimu wao waliona toka wanaingia shule walimu wao ni fimbo tu, ” amesema.

Mbali na suala la viboko, Naibu Katibu Mkuu  pia alizungumzia suala la kuwa na mikataba ya utendaji kazi kwa walimu.

Amesema serikali inataka kila mwalimu,kila msimamizi wa kazi ana mkataba wa utendaji kazi, lengo ni kuwapima walimu kutokana na mchango wao kwa nchi yao.

Naibu Katibu Mkuu ametaja vigezo vitatu vitakavyotumika kuwapima walimu hao kuwa ni pamoja na kuhakikisha kila mwalimu awe na mfumo wa kufundishia na kujifunzia, ambapo kila mwalimu atapaswa kuwa na azimio la kazi, mpango kazi lakini pia tunataka kuona mwalimu ana strategic plan (mpango mkakati) wa wapi anataka kuwapeleka watoto wake.

Wakati huo huo bwana Nzunda amesema kuwa serikali imetumia bilioni 29 kwa ajili ya kumalizia maboma yaliyokuwa yamejengwa na wananchi ili yakamilike na kutumika katika shule zetu.

Aidha Serikali sasa inajenga madarasa 2897 kwa shule za msingi kwa wakati mmoja na kuongeza kuwa serikali ya awamu ya tano inalenga kutumia raslimali kidogo kuleta matokeo makubwa.

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Waziri Jafo ataka Zimamoto, Skauti wakomeshe majanga ya moto shuleni

    February 26, 2021
  • Vikundi 13 Wilayani Kibaha vyanufaika na mikopo ya sh milioni 46

    February 25, 2021
  • Magufuli: Viongozi tatueni kero za wananchi kwa wakati

    February 25, 2021
  • Shilingi Bilioni 3 zakwamua Wanawake, Vijana na Walemavu Geita

    February 25, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.