• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya

Nzunda Aagiza Kuacha Vitendo vya Udanganyifu Mitihani Kidato cha Nne

Imewekwa tar.: November 13th, 2018


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI (ELIMU) Tixon Nzunda ametoa maagizo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri, Watendaji wa Elimu na Mamlaka za Elimu nchini kusimamia taaluma ili kumaliza tatizo la madawati na kudhibiti vitendo vya udanganyifu wakati wa mitihani.

Nzunda ametoa kauli hiyo alipotembelea shule ya sekondari ya wasichana Kibondo iliyopo wilayani Kibondo mkoani Kigoma ambapo amesema hivi karibuni kumekuwepo na vitendo vya udanganyifu katika mitihani kuanzia shule za msingi na sekondari jambo ambalo halitavumilika.

Nzunda amesema kuwa hatavumiliwa mtumishi yeyote yule atakayebainika kupokea rushwa na kufanya udanganyifu kwenye mitihani ikiwa ni pamoja na mitihani ya kidato cha nne inayoendelea hivi sasa nchini kote kwani kwa kufanya hivyo tunajenga Taifa la watu wasio na ushindani na wasio na maadili na wezi.

“katika mitihani ya kitaifa sitaki udanganyifu bali uadilifu, mtumishi yeyote atakaye jihusisha na udanganyifu na kubainika, huyo tutamwondoa katika Utumishi wa Umma, msifanye udanganyifu bali simamieni maadili”

Nzunda amesema tayari Maafisa Elimu4, Maafisa Taaluma 4, Waratibu Kata 19 na baadhi ya Wakuu wa shule wamechukuliwa hatua kwa kupatikana na hujuma katika mitihani nchini

Pia amewataka Maaafisa Elimu na Wakurugenzi nchini kuacha kuzalisha madeni mapya ya watumishi katika Mamlaka zao kwani kwa kufanya hivyo wanaipa Serikali mzigo mkubwa wa madeni jambo ambalo halitavumilika.

Katika ziara hiyo pia amewaagiza Maafisa Elimu na Wakurugenzi katika mikoa yenye miradi ya Equip pamoja na shule shikizi kuwa inahakikisha inamalizia miradi yote yakiwemo madarasa na madawati kwa wakati mara ili ifikapo januari, 2019 ili wanafunzi wote watakaochaguliwa kuingia kidato cha kwanza wanaanza masomo mara moja.

Mkuu wa shule hiyo Bi. Ruth Msweth ameishukuru Serikali kupitia mradi wake wa kukarabati shule kongwe nchini kuwa umeondoa changamoto lukuki zilizokuwa zinawakabili kama vile kuwepo kwa maji mpaka mabwenini, ujenzi wa madarasa na maabara mpya, ukarabatim wa miundo mbinu mingine na kuendelea kutenga bajeti ya elimu bila malipo kwani inasaidia kuendesha taaluma bila shida yoyote.

Naibu Katibu Mkuu Tixon Nzunda (ELIMU) Ofisi ya Rais TAMISEMI yupo mkoani Kigoma katika ziara yake ya kikazi akijionea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na miradi ya elimu na miradi ya kuboresha mazingira ya biashara (Local Investment Climate).

          Anaandika Fred Kibano


Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Wakurugenzi watakiwa kujitathimini Ukusanyaji wa Mapato

    January 21, 2021
  • Dodoma wapongezwa, wapewa miezi 5 kukamilisha ujenzi wa barabara

    January 20, 2021
  • Shule ya Msingi Nkuhungu yapewa siku 14 kukarabatiwa

    January 20, 2021
  • Asilimia 10 inavyoibua Wajasiriamali Arusha

    January 19, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.