• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App

Jafo- Nimeridhishwa na Mradi wa Utunzaji Mazingira

Imewekwa tar.: March 28th, 2019

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo, ameridhishwa na mradi wa utunzaji wa mazingira ulioanza unatekelezwa katika vijiji 30 wilayani Kilosa mkoani Morogoro, kwa ufadhili wa nchi ya Switzeland na kuiomba Serikali ya nchi hiyo kupitia kwa balozi wake nchini Florence Tinguely Mattli, kuona namna mradi huo utakavyo weza pelekwa maeneo mengine nchini.

Akizungumza ofisini kwake, wakati wa ugeni huo Mhe. Waziri amesema Serikali kupitia OR-TAMISEMI, wameridhishwa na jitihada hizo ambazo serikali ya nchi hiyo imezifanya katika kunusuru mazingira ya Wilaya za Mkoa wa Morogoro walizoanza anza nazo

“Katika mazungumzo yetu, tumekubaliana kwamba, sera zilizopo zinazohusu masuala ya mazingira lakini pia utunzaji wa misitu ya asili, wataalam kutoka OR-TAMISEMI kwakushirikiana na wataalam wengine wa wizara za kisekta kuzipitia na kuona kwa jinsi gani ni rafiki na zitaweza kutumika kuupeleka mradi huu sasa maeneo mengine ya nchi” alisema Waziri Jafo.

Waziri Jafo amesema kusudio la mradi huo kupitia Shirika la kuhifadhi Misitu ya Asili (Tanzania Forest Conservation Group-TFCG), umejielekeza katika misitu midogo midogo ya vijiji (Ngitiri) na  inayo milikiwa na Vijiji vyenyewe.

Mradi huo wa kuhifadhi Misitu ya Asili, ulianza mwaka 2012 katika Mkoa wa Morogoro, ulikuwa na awamu mbili ambapo katika awamu ya kwanza ilianza Machi, 2012 hadi Novemba, 2015, ikihusisha Vijiji 10 vya Halamashauri ya Wilaya ya Kilosa; na awamu ya Pili ilianza mwezi Desemba, 2015 kwa kuongezea Halmashauri za Wilaya ya Morogoro na Mvomero awamu inayotarajia kukamilika ifikiapo Novemba, 2019.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga kupitia taarifa yake aliyoitoa mbele ya Mhe. Waziri, inaonesha hadi sasa jumla ya Vijiji 30 vinatekeleza mradi huo kwenye Mkoa wa Morogoro ambapo Vijiji 20 vikiwa ni vya Wilaya ya Kilosa na Vijiji 10 katika Wilaya ya Morogoro.

Balozi wa Switzeland nchini Mhe. Florence Tinguely Mattli, alielezea kuridhishwa na juhudi zinazofanywa na Serikali ya awamu ya tano inayo ongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassani na wasaidizi wao wote.

Katika hatua nyingine Balozi huyo ameahidi kushirikiana na Tanzania katika suala shughuliza za sekta ya Afya husuan ni kwenye Afya katika Afya Msingi, ambapo alisema watakuwa tayari kuwezesha Vifaa tiba pamoja na eneo la TEHAMA. Kufuatia uamuzi huo Waziri wa Nchi amemuelekeza Katibu Mkuu OR-TAMISEMI Mhandisi Joseph Nyamhanga, kuwaita watendaji wa Ofisi hiyo wa Idara za Idara za TEHAMA pamoja na Huduma za Afya ili waweze kulisimamia.

Ujumbe wa Balozi wa Switzerland nchini ulimshukuru Mhe. Waziri kwa kutenga muda na kukutana nao ili kumuelezea dhamira waliyonayo katika suala zima la maendeleo ya nchi hususan ni katika sekta ya Afya na Mazingira nchini.  

Anaandika  Atley Kuni.



Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Kafanyeni Tohara kupunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi

    March 04, 2021
  • Uhaba wa Saruji wachelewesha ujenzi wa barabara za Mji wa Serikali

    March 03, 2021
  • Natoa siku siku 12 mtatue kero za soko la Ndugai na Stendi kuu ya Mabasi- Waziri Jafo

    March 03, 2021
  • Agizo la ujenzi wa vyumba vya madarasa 2257 latekelezwa

    March 02, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.