• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App

JAFO alia na riba kubwa za mikopo zinazotolewa na mabenki nchini

Imewekwa tar.: August 22nd, 2019

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe, Selemani Jafo amesema kuwa suala la mikopo wanayopewa waalimu na watu mbalimbali  nchini na  taasisi za kifedha zimekuwa ni  changamoto jambo ambalo linawasababisha kutokupata maendeleo stahiki na kuwa na madeni makubwa ambayo yanawasababishia umaskinii

Ameyasema hayo wakati akifungua siku wa waalimu kupitia benki ya NMB iliyofanyika leo katika ukumbi wa LAPF Jijini Dodoma.

Mhe. Jafo ameiomba benki ya NMB nchini kuhakikisha wanafanya utafiti wa kuwatambua wateja ambao ni wafanyakazi hasa Waalimu wanapatiwa mikopo yenye riba nafuu ambayo itawasaidia katika kujiongezea kipato na kujipatia maendeleo binafsi.

Ameendelea kufafanua kuwa benki hiyo inahitaji kuweka mikakati ya kuwasaidia waalimu pindi wanapokopa katika taasisi za kibenki kwa kuwapunguzia riba hadi kufikia digiti moja jambo ambalo litawafanya waalimu wengi kupata fursa ya kukopa na kujiendeleza kiuchumi.

Amesema lengo la mikopo ni kuwasaidia waalimu ili wajikwamue kiuchumi hivyo kwa kuweka riba kubwa kunasababisha waalimu wengi nchini kubaki maskini na kujikuta wanakopa kila mahali kutokana na fedha yote ya mshahara kuishia kwenye kulipa mikopo.

“Waalimu wakiajiriwa wanauhakika na ajira hiyo hadi kustaafu hivyo akikopa benki inauhakika na mteja huyo, sasa kwa nini riba ya mwalimu inakuwa sawasawa na mfanyabishara mkubwa au mfanyakazi ambaye ameajiriwa kwa mkataba, ninawaomba benki ya NMB mliangalie hilo ili waalimu wengi wajikwamue kiuchumi”Amesema  Mhe.Jafo

Amesema kuwa watumishi wengi wakiwemo waalimu wamekuwa wakiteseka na mikopo ambayo imekuwa ikitolewa na taasisi za kibenki jambo ambalo linasababisha malengo ya kufikia uchumi wa kati kuwa ni ndoto kwa watumishi wengi nchini.

“Ikifika tarehe 21 kila Mtumishi akiwemo mwalimu nchini kichwa kinamuuma kwa kuwa mshahara unakuwa umetoka lakini madeni aliyonayo yanazidi mshahara uliowekwa benki jambo ambalo linawafanya waalimu wengi kubaki maskini kila siku na kuwa watumwa wa mikopo” Amesema Mhe. Jafo.

Mhe. Jafo anafafanua kuwa Mikopo inawasaidia wananchi na hasa waalimu lakini bado wanateseka na riba kubwa zinazotolewa na mabenki jambo ambalo linawaumiza na kuwa watumwa wa kulipa madeni na sio kujikwamua kiuchumi.

Wakati huohuo Mhe. Jafo ametoa onyo kwa waalimu nchini kuacha kukopa mikopo kwa tamaa bali wakope kwa malengo ili kutimiza malengo yao ya kujiongezea kipato

“Waalimu wanaenda kukopa kwenye Sacoss hadi kadi zao za benki zinaachwa huko, mwalimu anatoa mpaka namba ya siri ya kadi yake ili mshahara ukiingie akatwe mkopo,hii si vizuri hata kidogo kwani waalimu wanadhalilika mitaani ” Amesema Mhe. Jafo.

Amewataka waalimu kuacha tamaa, bali waishi kulingana na kipato unachokipata, kwa kuwa kinachotokea baada ya kuwa na mikopo mingi ni waalimu wengi kudhalilika katika jamii

Aidha Mhe. Jafo ameitaka  benki ya NMB kuja na mkakati wa kuwasaidia waalimu katika kujikwamua kiuchumi na kujiongezea mapato lengo likiwa ni kupunguza umaskini nchini.

Na. Angela Msimbira OR-TAMISEMI




Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Agizo la ujenzi wa vyumba vya madarasa 2257 latekelezwa

    March 02, 2021
  • Waziri Jafo ataka Shilingi Bilioni 245 za Miradi ya Maendeleo zitumike kwa wakati

    March 01, 2021
  • Serikali yalegeza masharti mikopo ya asilimia 10

    February 27, 2021
  • Vikundi 23 Wilayani Busega vimenufaika na mikopo ya asilimia 10

    February 26, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.