• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App

Halmashauri zaagizwa kuitumia vizuri mifumo ya kielektroniki

Imewekwa tar.: June 11th, 2018

Na Mathew Kwembe, Kagera

Watendaji wa Halmashauri nchini wameagizwa kuitumia vizuri mifumo mbalimbali ya kielektroniki iliyowekwa na Serikali kwa kushirikiana na Mradi wa PS3 katika halmashauri zote 185 nchini ili mifumo hiyo iweze kufanya kazi yake kwa malengo yaliyokusudiwa.

Agizo hilo limetolewa leo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Kamishna wa Polisi Diwani Athuman wakati akifungua mafunzo ya siku nne ya Mfumo wa Epicor toleo la 10.2 kwa Waweka hazina, Wahasibu na Maafisa Wasimamizi wa Fedha kutoka Mikoa ya Mara na Kigoma yaliyofanyika mjini Bukoba.

Alisema kuwa mifumo hii imetumia fedha nyingi kuisimika na hivyo watendaji wa halmashauri hawana budi kulijua hilo na kuhakikisha kuwa wanaitumia katika kuboresha utendaji wao wa kazi na pia kuiwezesha serikali kutekeleza majukumu yake ya kuwahudumia wananchi.

Katibu Tawala huyo alisema kuwa ipo mifano kwa baadhi ya halmashauri katika mkoa wake ambazo watendaji wake wamekuwa wakishindwa kutekeleza majukumu yao vizuri.

Alisema kuwa halmashauri nyingi nchini zimewekewa mfumo wa ukusanyaji mapato lakini mifumo hii haitumiki kwa kiwango kilichokusudiwa.

Alisema halmashauri zimenunua vifaa vya kukusanyia mapato (POS) kwa ajili ya kuboresha ukusanyaji na kudhibiti udanganyifu na hila wakati ukusanyaji mapato lakini baadhi ya halmashauri zimeweka vifaa hivyo stoo.

Pia alisema kuwa uchunguzi walioufanya katika baadhi ya halmashauri za mkoa wake wamebaini kuwa baadhi ya watendaji wa halmashauri wasio waaminifu wamekuwa wakikusanya mapato kwa kutumia vifaa hivyo vya kielektroniki lakini fedha zinaishia mifukoni kwa watendaji hao.

“Mfano hapa Kagera tuna halmashauri ambazo pamoja na kuwekewa mifumo hii ya ukusanyaji mapato zimeshindwa kuitumia mifumo hiyo kukusanya mapato vizuri,” alieleza.

Akitolea mfano wa halmashauri ya wilaya ya Karagwe, Kamishna Athumani alisema kuwa uongozi wa mkoa wa Kagera umelazimika kutuma wataalamu kutoka taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa kwenda katika halmashauri hiyo ili kufanya uchunguzi wa uhakiki wa mifumo yao ya ukusanyaji mapato.

Hivyo Katibu Tawala huyo aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kutoka Mara na Kigoma kuhakikisha kuwa wanayatumia vizuri mafunzo hayo kwenda kuboresha utendaji wao wa kazi.

Aidha Kamishna Diwani aliwataka Wakurugenzi wa halmashauri nchini kuhakikisha kuwa wanatekeleza wajibu wao vizuri.

Alisema kuwa watendaji wa halmashauri hawana budi kujitafakari kama wanazitendea haki taaluma zao pale wanapotekeza majukumu yao kwani ni wajibu wao kuhakikisha kuwa wanatenda haki kwa umma kwa kutekeleza vizuri majukumu waliyopewa.

Kwa upande wake Meneja wa Mradi wa PS3 mkoa wa Kigoma Bwana Simon Mabagala alieleza kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo watendaji hao kutambua maboresho yaliyofanywa na serikali ya kuwa na mfumo mmoja wa usimamizi wa fedha za umma.

Mwakilishi wa washiriki wa mafunzo Bibi Mercy Swai ambaye ni Mwekahazina wa halmashauri ya Wilaya ya Kakonko kutoka mkoani Kigoma alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwao kwani yatawawezesha kumudu kuutumia mfumo wa Epicor ulioboreshwa.

Aliongeza kuwa matoleo yaliyopita yalikuwa na changamoto mbalimbali lakini mfumo wa Epicor toleo la 10.2 utawawezesha kuondokana na changamoto zilikuwepo katika mifumo iliyopita ya Epicor.



Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Kafanyeni Tohara kupunguza maambukizi ya virusi vya ukimwi

    March 04, 2021
  • Uhaba wa Saruji wachelewesha ujenzi wa barabara za Mji wa Serikali

    March 03, 2021
  • Natoa siku siku 12 mtatue kero za soko la Ndugai na Stendi kuu ya Mabasi- Waziri Jafo

    March 03, 2021
  • Agizo la ujenzi wa vyumba vya madarasa 2257 latekelezwa

    March 02, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.