• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Malalamiko |
    • Barua pepe za watumishi |
PO-RALG

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

  • Mwanzo
  • Utawala
  • Kuhusu Sisi
    • Local Government History
    • Kuhusu Wizara
      • Directories
    • Dira na Dhima
    • Majukumu ya Wizara
    • Mkataba wa Huduma kwa mteja
    • Idara
  • Mikoa
    • Arusha
    • Dar es Salaam
    • Dodoma
    • Geita
    • Iringa
    • Kigoma
    • Kilimanjaro
    • Lindi
    • Mbeya
    • Mara
    • Mtwara
    • Mwanza
    • Morogoro
    • Kagera
    • Manyara
    • Katavi
    • Pwani
    • Ruvuma
    • Rukwa
    • Shinyanga
    • Simiyu
    • Songwe
    • Tanga
    • Tabora
    • Njombe
    • Singida
  • Miradi na Programu
    • Tanzania Strategic Cities Project
    • MradiwaUendelezajiwaJiji la Dar es Salaam (DMDP)
    • Programu ya Miji Endeelevu (ULGSP)
    • Mradiwa Fursa na Vikwazo kwa Maendeleo (O &OD)
    • v. Mradi wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (Decentralized Climate Finance Project)
    • Programmu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP)
    • Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)
    • UNFPA
    • Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Wabunge (MP’s Office)
    • Mradiwa Ukarabati wa Vituo vya kutolea huduma za Afya
    • Primary school Development Plan
    • Secondary school Development Plan
    • Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
    • Programu ya kuzisaidia Serikali za Mitaa
    • Mpango wa Uboreshaji wa Mfumo wa Serikali za Mitaa
    • Mradi waujenzi wa Kituo cha Kumbukumbu za Serikali za Mitaa
    • Programu ya Uhamasishaji na Uchambuzi wa Sera
    • Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund)
    • LIC
    • Program (PFMRP)
    • Rural - Urban window
    • Mfumo wa kusajili Wajasiriamali Wadogo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Speech
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Machapisho ya Halmashauri
  • Machapisho
    • Taarifa Mbalimbali
    • Taarifa za Mapato
    • Majarida
    • Fomu Mbali mbali
    • Presentations
  • Miongozo
    • Miongozo OR TAMISEMI
    • Miongozo ya mradi wa SEQUIP
  • Vijiji na Miji
  • Nyaraka
    • Nyaraka za Elimu
    • Nyaraka za Afya
    • Fomu
    • SIS Mobile App

Dkt. Dugange, Awataka Watumishi Afya Wajitafakari wenyewe

Imewekwa tar.: December 11th, 2020

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (TAMISEMI) Mhe. Festo Dugange, anayeshughulikia Afya amewataka wataalam wa Afya katika ngazi za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kujitafakari na kubadilika ili kuendana na kasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli. Aidha kwa yeyote atakayeshindwa kufanya hivyo ni vema akawa tayari kupisha watu wenye uwezo.

Akizungumza kwenye kikao maalumu cha kujitambulisha mbele ya Watumishi wa Idara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ndani ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Dkt. Dugange, alisema, kutokana na mikakati iliyopo na mipango ya kusukuma sekta ya afya, nilazima kila mmoja ajitathimini kwa nafasi yake na majukumu aliyo nayo kama kweli anaitendea haki nafasi aliyo kabidhiwa.

Akiainisha vipaumbele muhimu Dkt. Dugange alisema, kubwa watakalo anza nalo ni uboresha wa upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi; uboreshaji wa mapato ametaja kama kipaumbele namba mbili huku akihimiza matumizi ya Mfumo wa GoTHOMIS, alisema suala la ukarabati mdogo mdogo kwenye vituo pamoja na maslahi na marupurupu ya watumishi yatategemea sana suala la uboreshaji wa mapato katika vyanzo vyote muhimu na hasa wakizingatia matumizi ya Mfumo.

“Katika ajenda hii ya mapato waganga wakuu wa Halmashauri wahakikishe baada ya tathmini ya ufatiliaji, yaonekane mabadiliko kwa macho ikiwepo vituo kupunguza utegemezi, ili kuweza kujifanyia baadhi ya mambo wao wenyewe”, alisema Dkt. Dugange na kuongeza kuwa, mbali ya boreshaji wa mapato vilevile ni lazima uboreshaji wa miundombinu iwe ni suala endelevu.

“Ni lazima pia tuboreshe miundombinu yetu na kuhakikisha ile asilimia ishirini ya ongezeko inayotajwa katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya 2020 hadi 2025, tunaifanyia kazi mapema kuanzia sasa kwa bajeti tulizo zipanga lakini pia kwakuwatumia wadau wetu wa maendeleo tunaoshirikiana nao, bila kusahau uhamasishaji wa jamii kuanza shughuli za ujenzi kama mpango wa jamii unavyo elekeza”. Alisema Naibu Waziri huyo.

Awali kabla ya kuzungumza na watumishi hao, Mkurugenzi wa Tiba na Ustawi wa Jamii, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Dkt. Ntuli Kapologwe, alimpongeza na kisha kutoa taarifa fupi ya utendaji kazi mbele ya Naibu Waziri huyo, ambapo pamoja na mambo mengine, Dkt. Ntuli alimuelezea Naibu Waziri juu ya ujenzi wa miundombinu ya afya katika ngazi mbali mbali.

“Sisi katika suala zima la miundombinu, ndani ya miaka mitano tumefanikiwa kujenga vituo 487 na kati ya hivyo 293 tayari vimeanza kutoa huduma na vingine vikiwa katika hatua mbalimbali, vile vile tumefanikiwa kusimamia ujenzi wa Hospitali za Halmashauri 102, ambapo 99 ni zile zilizojengwa kwa fedha za Serikali na Wadau na Halmashauri mbili za Nyamagana na Arusha hawa walijizatiti na wameweza kujenga wao wenyewe kwa mapato yao ya ndani, aidha jumla ya Zahanati 1,198 zimekamilika, lakini pia kuna baadhi ya Mikoa inayofanya jitihada binafsi ikiwepo Mkoa wa Geita ambao wapo katika mpango wa kujenga Zahanati 100.” Alisisitiza Dkt. Ntuli

Mbali na ujenzi huo pia Dkt. Ntuli alielezea suala la maboma ya Zahanati, yapatayo 555 katika mwaka wa fedha wa 2020/21, ambapo katika hali ya sasa lazima kila Halmashauri, iweze kufanya maombi ya fedha zenyewe, utaratibu huo ambao ni mpya una lengo la kuonesha hatua na juhudi binafasi kwa kila Halmashauri. Aidha taarifa hiyo imeonesha mbali ya Zahanati vipo pia vituo vya Afya 52 ambavyo vilipata Milioni. 200 kila kimoja na sasa kila Kituo kitalazimika kuongezewa Milioni. 300 kila kimoja ili waweza kufikisha jumla ya Milioni. 500 ili wakamilishe ujenzi na kuanza kutoa huduma.

Katika Hatua Nyingine Dkt. Ntuli, alimfafanulia, Naibu Waziri juu ya tafiti tunduizi na kubaini baadhi ya Hospitali za Wilaya kama Sengerema na Kahama,  ambazo zimekuwa zikipokea kina mama kwa ajili ya kujifungua wapatao 900 kila mwezi, hivyo ipo haja Hospitali hizo kuzipatiwa huduma za kibingwa kwani umbali wa Hospitali hizo na Makao Makuu zilipo Hospitali za Rufaa za Mikoa ni mbali.

“Mfano kwa Wilaya ya Kahama hadi Shinyanga Mjini ni zaidi ya Kilomita.102, hali inayochangia Vifo vya kina Mama kutokana na kusafirishwa umbali mrefu, kwa mantiki hiyo, tumeamua suala hili kuwapelekea wenzetu wa Wizara ya Afya, ili Hospitali hizi sasa ziweze kupewa hadhi ya Rufaa ya Mkoa na kupelekewa huduma za kibingwa”. Alisema Ntuli.

Dkt. Festo John Dugange, aliteuliwa kuwa Naibu Waziri anayeshughulikia Afya Ofisi ya Rais-TAMISEMI tarehe 05 Desemba, 2020 na kuapishwa tarehe 09 Desemba, 2020 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Ikulu ya Chamwino Dodoma.

Na. Atley Kuni-TAMISEMI, Dodoma

Mwisho.

Matangazo

  • Taarifa ya robo ya pili ya mapato ya Halmashauri, iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI January 21, 2021
  • Orodha ya majina ya matokeo ya kidato cha nne,cha pili na darasa la nne January 18, 2021
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2021 December 18, 2020
  • Michoro ya jengo la Ofisi za Halmashauri za Wilaya May 07, 2020
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIMU WALIOPANGWA KWENYE VITUO VYA KAZI NOVEMBA 2020 November 27, 2020
  • Orodha ya Vituo vya Afya na Zahanati vilivyo karabatiwa February 27, 2020
  • Angalia zote

Taarifa Mpya

  • Natoa siku siku 12 mtatue kero za soko la Ndugai na Stendi kuu ya Mabasi- Waziri Jafo

    March 03, 2021
  • Agizo la ujenzi wa vyumba vya madarasa 2257 latekelezwa

    March 02, 2021
  • Waziri Jafo ataka Shilingi Bilioni 245 za Miradi ya Maendeleo zitumike kwa wakati

    March 01, 2021
  • Serikali yalegeza masharti mikopo ya asilimia 10

    February 27, 2021
  • Angalia zote

Video

Tathmini Matokeo darasa la saba 2020
video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Miongozo ya OR TAMISEMI
  • Majarida Yetu
  • Wazo la Waziri
  • Maktaba ya picha
  • Fomu mbalimbali
  • Historia ya taasisi
  • Taarifa kwa Umma
  • Maktaba ya picha
  • TSCP kwa Undani
  • Uendelezaji Jiji la DSM DMDP
  • Uboreshaji wa Miji
  • Decentralised Climate Finance Project
  • O&OD Report
  • CAG Report
  • Habari mpya
  • Mfumo wa Kusajili Wajasiriamali Wadogo

Tovuti Muhimu

  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi ( LIVE)
  • Health System Strengthening Resource Center (HSSRC)
  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya Serikali
  • Wizara ya Afya
  • Ajira
  • Wizara ya Fedha
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tume ya Ajira Tanzania
  • Wizara ya Elimu

Waliotembelea kijiografia

world map hits counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

    S.L.P: 1923 Dodoma - Tanzania, Afrika Mashariki

    Simu: + 255 (26) 232 1 234

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ps@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

Imeanza Kuhesabu kuanzia Tar.27. Julai 2015
click here

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2018 Tamisemi. All rights reserved.